- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa AD 48–96
Letters to the Churches
Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.
Mistari ya kipindi hiki
- 1 Wakorintho 16:5takriban 59 BK
Baada ya kupitia Makedonia nitakuja kwenu, maana ninakusudia kupitia Makedonia.
- 1 Wakorintho 16:6takriban 59 BK
Huenda nitakaa nanyi kwa muda, au hata kukaa nanyi kipindi chote cha baridi, ili mweze kunisaidia katika safari yangu, popote niendapo.
- 1 Wakorintho 16:7takriban 59 BK
Kwa maana sitaki niwaone sasa na kupita tu; natarajia kuwa nanyi kwa muda wa kutosha, kama Bwana akipenda.
- 1 Wakorintho 16:8takriban 59 BK
Lakini nitakaa Efeso mpaka wakati wa Pentekoste,
- 1 Wakorintho 16:9takriban 59 BK
kwa maana mlango mkubwa umefunguliwa kwangu kufanya kazi yenye matunda, nako huko kuna adui wengi wanaonipinga.
- 1 Wakorintho 16:10takriban 59 BK
Ikiwa Timotheo atakuja kwenu, hakikisheni kwamba hana hofu yoyote akiwa nanyi, kwa sababu anafanya kazi ya Bwana, kama mimi nifanyavyo.
- 1 Wakorintho 16:11takriban 59 BK
Basi asiwepo mtu atakayekataa kumpokea. Msafirisheni kwa amani ili aweze kunijia tena. Namtarajia pamoja na ndugu.
- 1 Wakorintho 16:12takriban 59 BK
Basi kwa habari za ndugu yetu Apolo, nimemsihi kwa bidii aje kwenu pamoja na hao ndugu. Ingawa alikuwa hapendi kabisa kuja sasa, lakini atakuja apatapo nafasi.
- 1 Wakorintho 16:13takriban 59 BK
Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari.
- 1 Wakorintho 16:14takriban 59 BK
Fanyeni kila kitu katika upendo.
- 1 Wakorintho 16:15takriban 59 BK
Ninyi mnajua kwamba watu wa nyumbani mwa Stefana ndio waliokuwa wa kwanza kuamini katika Akaya, nao wamejitoa kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu. Ndugu nawasihi,
- 1 Wakorintho 16:16takriban 59 BK
mjitie katika kuwahudumia watu kama hawa na kila mmoja aingiaye kwenye kazi na kuifanya kwa bidii.
- 1 Wakorintho 16:17takriban 59 BK
Nilifurahi wakati Stefana, Fortunato na Akaiko walipofika, kwa sababu wamenipatia yale niliyopungukiwa kutoka kwenu.
- 1 Wakorintho 16:18takriban 59 BK
Kwa kuwa waliiburudisha roho yangu na zenu pia. Watu kama hawa wanastahili kutambuliwa.
- 1 Wakorintho 16:19takriban 59 BK
Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana.
- 1 Wakorintho 16:20takriban 59 BK
Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
- 1 Wakorintho 16:21takriban 59 BK
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.
- 1 Wakorintho 16:22takriban 59 BK
Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.
- 1 Wakorintho 16:23takriban 59 BK
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
- 1 Wakorintho 16:24takriban 59 BK
Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.
- 2 Wakorintho 1:1takriban 60 BK
Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
- 2 Wakorintho 1:2takriban 60 BK
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
- 2 Wakorintho 1:3takriban 60 BK
Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
- 2 Wakorintho 1:4takriban 60 BK
Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
- 2 Wakorintho 1:5takriban 60 BK
Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.