Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 2 Timotheo 1:1takriban 66 BK

    Paulo mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, kulingana na ile ahadi ya uzima uliomo ndani ya Kristo Yesu.

  2. 2 Timotheo 1:2takriban 66 BK

    Kwa Timotheo, mwanangu mpendwa: Neema, rehema na amani itokayo kwa Mungu Baba, na kwa Kristo Yesu Bwana wetu.

  3. 2 Timotheo 1:3takriban 66 BK

    Ninamshukuru Mungu, ninayemtumikia kwa dhamiri safi, kama walivyofanya baba zangu, ninapokukumbuka usiku na mchana katika maombi yangu.

  4. 2 Timotheo 1:4takriban 66 BK

    Nikiyakumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona ili nipate kujawa na furaha.

  5. 2 Timotheo 1:5takriban 66 BK

    Nimekuwa nikiikumbuka imani yako ya kweli, waliokuwa nayo bibi yako Loisi na mama yako Eunike na ambayo mimi ninasadiki sasa wewe pia unayo.

  6. 2 Timotheo 1:6takriban 66 BK

    Kwa sababu hii nakukumbusha uchochee ile karama ya Mungu, iliyowekwa ndani yako nilipokuwekea mikono yangu.

  7. 2 Timotheo 1:7takriban 66 BK

    Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali roho ya nguvu, ya upendo na ya moyo wa kiasi.

  8. 2 Timotheo 1:8takriban 66 BK

    Kwa hiyo usione haya kushuhudia kuhusu Bwana wetu, wala usinionee haya mimi niliye mfungwa kwa ajili yake. Bali uishiriki pamoja nami taabu ya Injili, kwa kadiri ya nguvu ya Mungu,

  9. 2 Timotheo 1:9takriban 66 BK

    ambaye alituokoa na kutuita katika mwito mtakatifu: si kwa kadiri ya matendo yetu mema bali kwa sababu ya kusudi lake mwenyewe na neema yake. Neema hii tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele.

  10. 2 Timotheo 1:10takriban 66 BK

    Lakini sasa imefunuliwa kwa kudhihirishwa kwake Mwokozi wetu, Kristo Yesu, ambaye amebatilisha mauti na kuleta uzima na kutokufa kwa njia ya Injili.

  11. 2 Timotheo 1:11takriban 66 BK

    Nami nimewekwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu wa Injili hii.

  12. 2 Timotheo 1:12takriban 66 BK

    Hii ndiyo sababu ninateseka namna hii, lakini sioni haya kwa maana ninamjua yeye niliyemwamini, na kusadiki ya kuwa anaweza kukilinda kile nilichokiweka amana kwake hadi siku ile.

  13. 2 Timotheo 1:13takriban 66 BK

    Shika kwa uthabiti kielelezo cha mafundisho yenye uzima yale uliyoyasikia kwangu, pamoja na imani na upendo katika Kristo Yesu.

  14. 2 Timotheo 1:14takriban 66 BK

    Ilinde ile amana uliyokabidhiwa kwa Roho Mtakatifu akaaye ndani yetu.

  15. 2 Timotheo 1:15takriban 66 BK

    Unajua ya kuwa watu wote katika Asia wameniacha, miongoni mwao wamo Filego na Hermogene.

  16. 2 Timotheo 1:16takriban 66 BK

    Bwana akawahurumie watu wa nyumbani mwa Onesiforo, kwa sababu aliniburudisha mara kwa mara wala hakuionea aibu minyororo yangu.

  17. 2 Timotheo 1:17takriban 66 BK

    Badala yake, alipokuwa Rumi, alinitafuta kwa bidii mpaka akanipata.

  18. 2 Timotheo 1:18takriban 66 BK

    Bwana na amjalie kupata rehema zake siku ile! Nawe unajua vyema jinsi alivyonisaidia huko Efeso.

  19. 2 Timotheo 2:1takriban 66 BK

    Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.

  20. 2 Timotheo 2:2takriban 66 BK

    Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.

  21. 2 Timotheo 2:3takriban 66 BK

    Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.

  22. 2 Timotheo 2:4takriban 66 BK

    Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.

  23. 2 Timotheo 2:5takriban 66 BK

    Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.

  24. 2 Timotheo 2:6takriban 66 BK

    Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.

  25. 2 Timotheo 2:7takriban 66 BK

    Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.