Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 2 Wathesalonike 1:1takriban 54 BK

    Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:

  2. 2 Wathesalonike 1:2takriban 54 BK

    Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

  3. 2 Wathesalonike 1:3takriban 54 BK

    Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.

  4. 2 Wathesalonike 1:4takriban 54 BK

    Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.

  5. 2 Wathesalonike 1:5takriban 54 BK

    Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.

  6. 2 Wathesalonike 1:6takriban 54 BK

    Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi

  7. 2 Wathesalonike 1:7takriban 54 BK

    na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.

  8. 2 Wathesalonike 1:8takriban 54 BK

    Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.

  9. 2 Wathesalonike 1:9takriban 54 BK

    Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake,

  10. 2 Wathesalonike 1:10takriban 54 BK

    siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.

  11. 2 Wathesalonike 1:11takriban 54 BK

    Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.

  12. 2 Wathesalonike 1:12takriban 54 BK

    Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.

  13. 2 Wathesalonike 2:1takriban 54 BK

    Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,

  14. 2 Wathesalonike 2:2takriban 54 BK

    msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.

  15. 2 Wathesalonike 2:3takriban 54 BK

    Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.

  16. 2 Wathesalonike 2:4takriban 54 BK

    Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.

  17. 2 Wathesalonike 2:5takriban 54 BK

    Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?

  18. 2 Wathesalonike 2:6takriban 54 BK

    Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.

  19. 2 Wathesalonike 2:7takriban 54 BK

    Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.

  20. 2 Wathesalonike 2:8takriban 54 BK

    Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.

  21. 2 Wathesalonike 2:9takriban 54 BK

    Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,

  22. 2 Wathesalonike 2:10takriban 54 BK

    na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.

  23. 2 Wathesalonike 2:11takriban 54 BK

    Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,

  24. 2 Wathesalonike 2:12takriban 54 BK

    na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.

  25. 2 Wathesalonike 2:13takriban 54 BK

    Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.