Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 1:1takriban 59 BK

    Paulo, niliyeitwa kwa mapenzi ya Mungu kuwa mtume wa Kristo Yesu, na Sosthene ndugu yetu.

  2. 1 Wakorintho 1:2takriban 59 BK

    Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale waliotakaswa katika Kristo Yesu na walioitwa kuwa watakatifu, pamoja na wale wote ambao kila mahali wanaliitia Jina la Kristo Yesu Bwana wetu, aliye Bwana wao na wetu pia:

  3. 1 Wakorintho 1:3takriban 59 BK

    Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.

  4. 1 Wakorintho 1:4takriban 59 BK

    Ninamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu kwa sababu ya neema yake mliyopewa katika Kristo Yesu.

  5. 1 Wakorintho 1:5takriban 59 BK

    Kwa kuwa katika Kristo mmetajirishwa kwa kila hali, katika kusema kwenu na katika maarifa yenu yote,

  6. 1 Wakorintho 1:6takriban 59 BK

    kwa sababu ushuhuda wetu kumhusu Kristo ulithibitishwa ndani yenu.

  7. 1 Wakorintho 1:7takriban 59 BK

    Kwa hiyo hamkupungukiwa na karama yoyote ya kiroho wakati mnangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

  8. 1 Wakorintho 1:8takriban 59 BK

    Atawafanya imara mpaka mwisho, ili msiwe na hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.

  9. 1 Wakorintho 1:9takriban 59 BK

    Mungu ambaye mmeitwa naye ili mwe na ushirika na Mwanawe Yesu Kristo, Bwana wetu ni mwaminifu.

  10. 1 Wakorintho 1:10takriban 59 BK

    Nawasihi ndugu zangu, katika Jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi, ili pasiwepo na matengano katikati yenu na kwamba mwe na umoja kikamilifu katika nia na katika kusudi.

  11. 1 Wakorintho 1:11takriban 59 BK

    Ndugu zangu, nimepata habari kutoka kwa baadhi ya watu wa nyumbani mwa Kloe kwamba kuna magomvi katikati yenu.

  12. 1 Wakorintho 1:12takriban 59 BK

    Maana yangu ni kwamba: Mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo”; mwingine, “Mimi ni wa Apolo”; mwingine, “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine, “Mimi ni wa Kristo.”

  13. 1 Wakorintho 1:13takriban 59 BK

    Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye alisulubishwa kwa ajili yenu? Je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?

  14. 1 Wakorintho 1:14takriban 59 BK

    Nashukuru kwamba sikumbatiza mtu yeyote isipokuwa Krispo na Gayo.

  15. 1 Wakorintho 1:15takriban 59 BK

    Kwa hiyo hakuna mtu yeyote anayeweza kusema kwamba alibatizwa kwa jina langu.

  16. 1 Wakorintho 1:16takriban 59 BK

    (Naam, niliwabatiza pia watu wa nyumbani mwa Stefana. Lakini zaidi ya hao sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)

  17. 1 Wakorintho 1:17takriban 59 BK

    Kwa maana Kristo hakunituma ili kubatiza bali kuhubiri Injili; sio kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili msalaba wa Kristo usije ukakosa nguvu yake.

  18. 1 Wakorintho 1:18takriban 59 BK

    Kwa maana ujumbe wa msalaba kwa wale wanaopotea ni upuzi, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.

  19. 1 Wakorintho 1:19takriban 59 BK

    Kwa maana imeandikwa: “Nitaiharibu hekima ya wenye hekima, na kubatilisha akili ya wenye akili.”

  20. 1 Wakorintho 1:20takriban 59 BK

    Yuko wapi mwenye hekima? Yuko wapi msomi? Yuko wapi mwanafalsafa wa nyakati hizi? Je, Mungu hakufanya hekima ya ulimwengu huu kuwa upumbavu?

  21. 1 Wakorintho 1:21takriban 59 BK

    Kwa kuwa katika hekima ya Mungu, ulimwengu kwa hekima yake haukumjua yeye, ilimpendeza Mungu kuwaokoa wale walioamini kwa upuzi wa lile neno lililohubiriwa.

  22. 1 Wakorintho 1:22takriban 59 BK

    Wayahudi wanadai ishara za miujiza na Wayunani wanatafuta hekima.

  23. 1 Wakorintho 1:23takriban 59 BK

    Lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa: yeye kwa Wayahudi ni kikwazo na kwa Wayunani ni upuzi.

  24. 1 Wakorintho 1:24takriban 59 BK

    Lakini kwa wale ambao Mungu amewaita, Wayahudi na pia Wayunani, Kristo ndiye nguvu ya Mungu na pia hekima ya Mungu.

  25. 1 Wakorintho 1:25takriban 59 BK

    Kwa maana upumbavu wa Mungu una hekima zaidi kuliko hekima ya wanadamu, nao udhaifu wa Mungu una nguvu kuliko nguvu ya wanadamu.