Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Waefeso 1:1takriban 64 BK

    Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu: Kwa watakatifu walioko Efeso, walio waaminifu katika Kristo Yesu:

  2. Waefeso 1:2takriban 64 BK

    Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.

  3. Waefeso 1:3takriban 64 BK

    Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki sisi kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho ndani ya Kristo.

  4. Waefeso 1:4takriban 64 BK

    Kwa maana alituchagua katika yeye kabla ya kuumbwa ulimwengu ili tuwe watakatifu na bila lawama mbele zake. Kwa upendo

  5. Waefeso 1:5takriban 64 BK

    alitangulia kutuchagua tuwe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo kwa furaha yake na mapenzi yake mwenyewe.

  6. Waefeso 1:6takriban 64 BK

    Kwa hiyo tunamsifu Mungu kwa huruma zake kuu alizotumiminia sisi katika Mwanawe Mpendwa.

  7. Waefeso 1:7takriban 64 BK

    Ndani yake tunao ukombozi kwa njia ya damu yake, yaani, msamaha wa dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake

  8. Waefeso 1:8takriban 64 BK

    aliyotumiminia kwa wingi, kwa hekima yote na maarifa yote.

  9. Waefeso 1:9takriban 64 BK

    Naye alitujulisha siri ya mapenzi yake sawasawa na uradhi wa mapenzi yake, ambayo alikusudia katika Kristo,

  10. Waefeso 1:10takriban 64 BK

    ili yapate kutimizwa wakati mkamilifu utakapowadia, yaani, kuvitia vitu vyote vya mbinguni na vya duniani pamoja, chini ya kiongozi mmoja, ndiye Kristo.

  11. Waefeso 1:11takriban 64 BK

    Katika Kristo sisi nasi tumepata urithi, tukisha kuchaguliwa sawasawa na kusudi la Mungu, yeye ambaye hufanya mambo yote kulingana na kusudi la mapenzi yake,

  12. Waefeso 1:12takriban 64 BK

    ili kwamba, sisi tuliokuwa wa kwanza kuweka tumaini katika Kristo, tupate kuishi kwa sifa ya utukufu wake.

  13. Waefeso 1:13takriban 64 BK

    Ninyi pia mliingia ndani ya Kristo mliposikia Neno la kweli, Injili ya wokovu wenu. Mkiisha kuamini, ndani yake mlitiwa muhuri, yaani, Roho Mtakatifu mliyeahidiwa,

  14. Waefeso 1:14takriban 64 BK

    yeye ambaye ni amana yetu akituhakikishia urithi wetu hadi ukombozi wa wale walio milki ya Mungu kwa sifa ya utukufu wake.

  15. Waefeso 1:15takriban 64 BK

    Kwa sababu hii, tangu niliposikia juu ya imani yenu katika Bwana Yesu na upendo wenu kwa watakatifu wote,

  16. Waefeso 1:16takriban 64 BK

    sijaacha kumshukuru Mungu kwa ajili yenu, nikiwakumbuka katika maombi yangu.

  17. Waefeso 1:17takriban 64 BK

    Nazidi kumwomba Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awajalieni ninyi roho ya hekima na ya ufunuo, ili mpate kumjua zaidi.

  18. Waefeso 1:18takriban 64 BK

    Ninaomba pia kwamba macho ya mioyo yenu yatiwe nuru ili mpate kujua tumaini mliloitiwa, utajiri wa urithi wa utukufu wake kwa watakatifu

  19. Waefeso 1:19takriban 64 BK

    na uweza wake mkuu usiolinganishwa kwa ajili yetu sisi tuaminio. Uweza huo unaofanya kazi ndani yetu, ni sawa na ile nguvu kuu mno

  20. Waefeso 1:20takriban 64 BK

    aliyoitumia katika Kristo alipomfufua kutoka kwa wafu, na akamketisha mkono wake wa kuume huko mbinguni,

  21. Waefeso 1:21takriban 64 BK

    juu sana kuliko falme zote na mamlaka, enzi na milki, na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu, bali katika ule ujao pia.

  22. Waefeso 1:22takriban 64 BK

    Naye Mungu ameweka vitu vyote viwe chini ya miguu yake na amemfanya yeye awe kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya Kanisa,

  23. Waefeso 1:23takriban 64 BK

    ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake yeye aliye yote katika yote.

  24. Waefeso 2:1takriban 64 BK

    Kwa habari zenu, mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu,

  25. Waefeso 2:2takriban 64 BK

    ambazo mlizitenda mlipofuatisha namna ya ulimwengu huu na za yule mtawala wa ufalme wa anga, yule roho atendaye kazi sasa ndani ya wale wasiotii.