Rukia maudhui

circa 1406–1380 BC

Conquest of Canaan

Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.

658 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Yoshua 19:31takriban 1443 KK

    Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.

  2. Yoshua 19:32takriban 1443 KK

    Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:

  3. Yoshua 19:33takriban 1443 KK

    Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.

  4. Yoshua 19:34takriban 1443 KK

    Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.

  5. Yoshua 19:35takriban 1443 KK

    Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,

  6. Yoshua 19:36takriban 1443 KK

    Adama, Rama, Hazori,

  7. Yoshua 19:37takriban 1443 KK

    Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,

  8. Yoshua 19:38takriban 1443 KK

    Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.

  9. Yoshua 19:39takriban 1443 KK

    Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.

  10. Yoshua 19:40takriban 1443 KK

    Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.

  11. Yoshua 19:41takriban 1443 KK

    Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,

  12. Yoshua 19:42takriban 1443 KK

    Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,

  13. Yoshua 19:43takriban 1443 KK

    Eloni, Timna, Ekroni,

  14. Yoshua 19:44takriban 1443 KK

    Elteke, Gibethoni, Baalathi,

  15. Yoshua 19:45takriban 1443 KK

    Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,

  16. Yoshua 19:46takriban 1443 KK

    Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.

  17. Yoshua 19:47takriban 1443 KK

    (Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)

  18. Yoshua 19:48takriban 1443 KK

    Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.

  19. Yoshua 19:49takriban 1443 KK

    Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,

  20. Yoshua 19:50takriban 1443 KK

    kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.

  21. Yoshua 19:51takriban 1443 KK

    Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

  22. Yoshua 20:1takriban 1443 KK

    Ndipo Bwana akamwambia Yoshua,

  23. Yoshua 20:2takriban 1443 KK

    “Waambie Waisraeli, watenge miji mikubwa ya kukimbilia, kama nilivyokuagiza kupitia Mose,

  24. Yoshua 20:3takriban 1443 KK

    ili mtu yeyote atakayemuua mtu kwa bahati mbaya na pasipo kukusudia aweze kukimbilia huko na kujiepusha na mlipiza kisasi wa damu.

  25. Yoshua 20:4takriban 1443 KK

    “Anapokimbilia mojawapo ya hii miji mikubwa atasimama kwenye maingilio ya lango la mji mkuu na kueleza wazee wa mji kuhusu shauri lake. Kisha watampokea katika mji wao na kumpa mahali pa kuishi nao.