Skip to content

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hesabu 1:1takriban 1490 KK

    Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,

  2. Hesabu 1:2takriban 1490 KK

    “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.

  3. Hesabu 1:3takriban 1490 KK

    Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.

  4. Hesabu 1:4takriban 1490 KK

    Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.

  5. Hesabu 1:5takriban 1490 KK

    Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;

  6. Hesabu 1:6takriban 1490 KK

    kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;

  7. Hesabu 1:7takriban 1490 KK

    kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;

  8. Hesabu 1:8takriban 1490 KK

    kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;

  9. Hesabu 1:9takriban 1490 KK

    kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;

  10. Hesabu 1:10takriban 1490 KK

    kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;

  11. Hesabu 1:11takriban 1490 KK

    kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;

  12. Hesabu 1:12takriban 1490 KK

    kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;

  13. Hesabu 1:13takriban 1490 KK

    kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;

  14. Hesabu 1:14takriban 1490 KK

    kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;

  15. Hesabu 1:15takriban 1490 KK

    kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”

  16. Hesabu 1:16takriban 1490 KK

    Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.

  17. Hesabu 1:17takriban 1490 KK

    Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,

  18. Hesabu 1:18takriban 1490 KK

    wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,

  19. Hesabu 1:19takriban 1490 KK

    kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:

  20. Hesabu 1:20takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  21. Hesabu 1:21takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.

  22. Hesabu 1:22takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  23. Hesabu 1:23takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.

  24. Hesabu 1:24takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  25. Hesabu 1:25takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.