Rukia maudhui

circa 1446–1406 BC

The Wilderness Years

Forty years of wandering in the desert test Israel's faith and prepare a new generation to enter the promised land.

2,247 mistari · 2 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hesabu 1:26takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  2. Hesabu 1:27takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.

  3. Hesabu 1:28takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  4. Hesabu 1:29takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.

  5. Hesabu 1:30takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  6. Hesabu 1:31takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.

  7. Hesabu 1:32takriban 1490 KK

    Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  8. Hesabu 1:33takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.

  9. Hesabu 1:34takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  10. Hesabu 1:35takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.

  11. Hesabu 1:36takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  12. Hesabu 1:37takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.

  13. Hesabu 1:38takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  14. Hesabu 1:39takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.

  15. Hesabu 1:40takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  16. Hesabu 1:41takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.

  17. Hesabu 1:42takriban 1490 KK

    Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.

  18. Hesabu 1:43takriban 1490 KK

    Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.

  19. Hesabu 1:44takriban 1490 KK

    Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.

  20. Hesabu 1:45takriban 1490 KK

    Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.

  21. Hesabu 1:46takriban 1490 KK

    Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.

  22. Hesabu 1:47takriban 1490 KK

    Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.

  23. Hesabu 1:48takriban 1490 KK

    Bwana alikuwa amemwambia Mose:

  24. Hesabu 1:49takriban 1490 KK

    “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.

  25. Hesabu 1:50takriban 1490 KK

    Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.