Rukia maudhui

circa 1406–1380 BC

Conquest of Canaan

Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.

658 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Yoshua 21:21takriban 1443 KK

    Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,

  2. Yoshua 21:22takriban 1443 KK

    Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

  3. Yoshua 21:23takriban 1443 KK

    Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,

  4. Yoshua 21:24takriban 1443 KK

    Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne

  5. Yoshua 21:25takriban 1443 KK

    Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.

  6. Yoshua 21:26takriban 1443 KK

    Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.

  7. Yoshua 21:27takriban 1443 KK

    Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;

  8. Yoshua 21:28takriban 1443 KK

    kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,

  9. Yoshua 21:29takriban 1443 KK

    Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne

  10. Yoshua 21:30takriban 1443 KK

    kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,

  11. Yoshua 21:31takriban 1443 KK

    Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

  12. Yoshua 21:32takriban 1443 KK

    Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.

  13. Yoshua 21:33takriban 1443 KK

    Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.

  14. Yoshua 21:34takriban 1443 KK

    Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,

  15. Yoshua 21:35takriban 1443 KK

    Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;

  16. Yoshua 21:36takriban 1443 KK

    kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,

  17. Yoshua 21:37takriban 1443 KK

    Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;

  18. Yoshua 21:38takriban 1443 KK

    kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,

  19. Yoshua 21:39takriban 1443 KK

    Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.

  20. Yoshua 21:40takriban 1443 KK

    Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.

  21. Yoshua 21:41takriban 1443 KK

    Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.

  22. Yoshua 21:42takriban 1443 KK

    Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.

  23. Yoshua 21:43takriban 1443 KK

    Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.

  24. Yoshua 21:44takriban 1443 KK

    Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.

  25. Yoshua 21:45takriban 1443 KK

    Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.