Rukia maudhui

circa 1406–1380 BC

Conquest of Canaan

Joshua leads Israel across the Jordan into the promised land, defeating the Canaanite kingdoms one by one.

658 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Yoshua 18:9takriban 1443 KK

    Ndipo hao watu walipoondoka na kupita katika ile nchi. Wakaandika maelezo yake kwenye kitabu, mji kwa mji, katika sehemu saba na kurudisha taarifa kwa Yoshua huko kambini Shilo.

  2. Yoshua 18:10takriban 1443 KK

    Basi Yoshua akawapigia kura huko Shilo mbele za Bwana, na hapo akagawanya ile nchi kwa Waisraeli kufuatana na mgawanyo wa kabila zao.

  3. Yoshua 18:11takriban 1443 KK

    Kura iliangukia kabila la Benyamini, ukoo kwa ukoo. Eneo lao walilogawiwa lilikuwa kati ya kabila la Yuda na la Yosefu.

  4. Yoshua 18:12takriban 1443 KK

    Upande wa kaskazini mpaka wao ulianzia pale Yordani, kupitia kaskazini ya mteremko wa Yeriko na kuendelea magharibi kuingia katika nchi ya vilima, ukitokea kwenye jangwa la Beth-Aveni.

  5. Yoshua 18:13takriban 1443 KK

    Kutoka hapo ulikatiza kwenye mteremko wa kusini mwa Luzu (yaani Betheli) na kushuka hadi Ataroth-Adari katika kilima kusini mwa Beth-Horoni ya Chini.

  6. Yoshua 18:14takriban 1443 KK

    Kutoka kilima kinachotazamana na Beth-Horoni upande wa kusini mpaka ule ukazunguka kusini kufuatia upande wa magharibi, na ukatokezea Kiriath-Baali (yaani Kiriath-Yearimu), mji wa watu wa Yuda. Huu ndio uliokuwa upande wa magharibi.

  7. Yoshua 18:15takriban 1443 KK

    Upande wa kusini mpaka ulianzia kwenye viunga vya Kiriath-Yearimu kwa upande wa magharibi, nao ukatokeza kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa.

  8. Yoshua 18:16takriban 1443 KK

    Mpaka ukateremka hadi shefela inayotazamana na Bonde la Ben-Hinomu, kaskazini mwa Bonde la Refaimu. Ukaendelea chini kwenye Bonde la Hinomu sambamba na mteremko wa kusini mwa mji mkubwa wa Wayebusi na kisha hadi En-Rogeli.

  9. Yoshua 18:17takriban 1443 KK

    Kisha ukapinda kuelekea kaskazini, ukaenda hadi En-Shemeshi na kuendelea mpaka Gelilothi, inayotazamana na Njia ya Adumimu, ukateremka hadi kwenye Jiwe la Bohani mwana wa Reubeni.

  10. Yoshua 18:18takriban 1443 KK

    Ukaendelea upande wa mteremko wa kaskazini wa Beth-Araba ukateremka hadi Araba.

  11. Yoshua 18:19takriban 1443 KK

    Kisha ukaenda mpaka kwenye mteremko wa kaskazini wa Beth-Hogla na kujitokeza kwenye ghuba ya kaskazini ya Bahari ya Chumvi, kwenye maingilio ya Yordani upande wa kusini. Huo ulikuwa mpaka wa kusini.

  12. Yoshua 18:20takriban 1443 KK

    Nayo Yordani ikawa ndio mpaka wa upande wa mashariki. Hii ilikuwa ndiyo mipaka iliyoonyesha urithi wa koo za Benyamini pande zote.

  13. Yoshua 18:21takriban 1443 KK

    Kabila ya Benyamini, ukoo kwa ukoo, ilikuwa na miji mikubwa ifuatayo: Yeriko, Beth-Hogla, Emeki-Kesisi,

  14. Yoshua 18:22takriban 1443 KK

    Beth-Araba, Semaraimu, Betheli,

  15. Yoshua 18:23takriban 1443 KK

    Avimu, Para na Ofra,

  16. Yoshua 18:24takriban 1443 KK

    Kefar-Amoni, Ofni, na Geba; miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.

  17. Yoshua 18:25takriban 1443 KK

    Gibeoni, Rama na Beerothi,

  18. Yoshua 18:26takriban 1443 KK

    Mispa, Kefira, Moza,

  19. Yoshua 18:27takriban 1443 KK

    Rekemu, Irpeeli, Tarala,

  20. Yoshua 18:28takriban 1443 KK

    Zela, Elefu, mji wa Wayebusi (yaani Yerusalemu), Gibea na Kiriathi; miji kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Huu ndio uliokuwa urithi wa Benyamini kwa ajili ya koo zake.

  21. Yoshua 19:1takriban 1443 KK

    Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.

  22. Yoshua 19:2takriban 1443 KK

    Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,

  23. Yoshua 19:3takriban 1443 KK

    Hasar-Shuali, Bala, Esemu,

  24. Yoshua 19:4takriban 1443 KK

    Eltoladi, Bethuli, Horma,

  25. Yoshua 19:5takriban 1443 KK

    Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,