Rukia maudhui

Creation Era

The Tower of Babel

Scattered nations and confused languages mark the beginning of the diversity of peoples across the earth.

64 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Mwanzo 10:26takriban 2247 KK

    Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,

  2. Mwanzo 10:27takriban 2247 KK

    Hadoramu, Uzali, Dikla,

  3. Mwanzo 10:28takriban 2207 KK

    Obali, Abimaeli, Sheba,

  4. Mwanzo 10:29takriban 2207 KK

    Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.

  5. Mwanzo 10:30takriban 2207 KK

    Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.

  6. Mwanzo 10:31takriban 2207 KK

    Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.

  7. Mwanzo 10:32takriban 2207 KK

    Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

  8. Mwanzo 11:1takriban 2247 KK

    Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.

  9. Mwanzo 11:2takriban 2247 KK

    Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.

  10. Mwanzo 11:3takriban 2247 KK

    Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.

  11. Mwanzo 11:4takriban 2247 KK

    Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”

  12. Mwanzo 11:5takriban 2247 KK

    Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.

  13. Mwanzo 11:6takriban 2247 KK

    Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.

  14. Mwanzo 11:7takriban 2247 KK

    Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”

  15. Mwanzo 11:8takriban 2247 KK

    Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.

  16. Mwanzo 11:9takriban 2247 KK

    Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.

  17. Mwanzo 11:10takriban 2346 KK

    Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.

  18. Mwanzo 11:11takriban 1846 KK

    Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  19. Mwanzo 11:12takriban 2311 KK

    Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.

  20. Mwanzo 11:13takriban 1908 KK

    Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  21. Mwanzo 11:14takriban 2281 KK

    Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.

  22. Mwanzo 11:15takriban 1878 KK

    Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  23. Mwanzo 11:16takriban 2247 KK

    Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.

  24. Mwanzo 11:17takriban 1817 KK

    Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.

  25. Mwanzo 11:18takriban 2217 KK

    Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.