Skip to content

Creation Era

The Great Flood

Humanity's wickedness fills the earth; God preserves Noah and his family through a catastrophic flood.

97 mistari · 1 kitabu kimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

  1. Mwanzo 6:1takriban 2448 KK

    Watu walipoanza kuongezeka idadi katika uso wa dunia na watoto wa kike wakazaliwa kwao,

  2. Mwanzo 6:2takriban 2448 KK

    wana wa Mungu wakawaona kuwa hao binti za wanadamu walikuwa wazuri wa sura, wakaoa yeyote miongoni mwao waliyemchagua.

  3. Mwanzo 6:3takriban 2448 KK

    Ndipo Bwana akasema, “Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye ni wa kufa, siku zake zitakuwa miaka 120.”

  4. Mwanzo 6:4takriban 2448 KK

    Wanefili walikuwako duniani siku hizo, na baadaye, hao wana wa Mungu walipoingia kwa binti za wanadamu na kuzaa nao. Wanefili walikuwa mashujaa na watu waliojulikana wa zamani hizo.

  5. Mwanzo 6:5takriban 2448 KK

    Bwana akaona jinsi uovu wa mwanadamu ulivyokuwa mkubwa duniani, na ya kuwa kila mwelekeo wa mawazo ya moyo wake wakati wote ulikuwa mbaya tu.

  6. Mwanzo 6:6takriban 2448 KK

    Bwana akasikitika kwamba alimuumba mwanadamu duniani, moyo wa Mungu ukajaa masikitiko.

  7. Mwanzo 6:7takriban 2448 KK

    Kwa hiyo Bwana akasema, “Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemuumba kutoka kwenye uso wa dunia, wanadamu na wanyama, pamoja na viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Kwa maana nasikitika kuwaumba.”

  8. Mwanzo 6:8takriban 2448 KK

    Lakini Noa akapata kibali machoni pa Bwana.

  9. Mwanzo 6:9takriban 2448 KK

    Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.

  10. Mwanzo 6:10takriban 2448 KK

    Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.

  11. Mwanzo 6:11takriban 2448 KK

    Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.

  12. Mwanzo 6:12takriban 2448 KK

    Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.

  13. Mwanzo 6:13takriban 2448 KK

    Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.

  14. Mwanzo 6:14takriban 2468 KK

    Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.

  15. Mwanzo 6:15takriban 2468 KK

    Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.

  16. Mwanzo 6:16takriban 2468 KK

    Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.

  17. Mwanzo 6:17takriban 2468 KK

    Nitaleta gharika ya maji juu ya nchi ili kuangamiza uhai wote chini ya mbingu, kila kiumbe chenye pumzi ya uhai ndani yake. Kila kitu juu ya nchi kitaangamia.

  18. Mwanzo 6:18takriban 2468 KK

    Lakini Mimi nitaweka Agano langu na wewe, nawe utaingia ndani ya Safina, wewe pamoja na mke wako, wanao na wake zao.

  19. Mwanzo 6:19takriban 2468 KK

    Utaingiza ndani ya Safina kila aina ya kiumbe hai wawili wawili, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja na wewe.

  20. Mwanzo 6:20takriban 2468 KK

    Wawili wa kila aina ya ndege, wa kila aina ya mnyama na wa kila aina ya kitambaacho ardhini watakuja kwako ili wahifadhiwe hai.

  21. Mwanzo 6:21takriban 2468 KK

    Utachukua kila aina ya chakula kitakacholiwa, na ukiweke akiba kama chakula kwa ajili yako na yao.”

  22. Mwanzo 6:22takriban 2468 KK

    Noa akafanya kila kitu kama vile Mungu alivyomwamuru.

  23. Mwanzo 7:1takriban 2348 KK

    Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.

  24. Mwanzo 7:2takriban 2348 KK

    Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.

  25. Mwanzo 7:3takriban 2348 KK

    Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.