Skip to content

Ham

14 mistari · 7 wanafamilia

Mistari inayomtaja Ham

  1. Baada ya Noa kuishi miaka 500, aliwazaa Shemu, Hamu na Yafethi.

  2. Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.

  3. Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.

  4. Wana wa Noa waliotoka ndani ya safina ni: Shemu, Hamu na Yafethi. (Hamu ndiye alikuwa baba wa Kanaani.)

  5. Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake na kuwaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.

  6. Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.

  7. Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.

  8. Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.

  9. Wana wa Noa walikuwa: Shemu, Hamu na Yafethi.

  10. Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.

  11. Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu.

  12. Kisha Israeli akaingia Misri, Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.

  13. Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao, miujiza yake katika nchi ya Hamu.

  14. miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.