Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Sciences

74 mistari · 13 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Kwa hiyo jitengenezee safina kubwa kwa mbao za mvinje, tengeneza vyumba ndani yake na uipake lami ndani na nje.

  2. Hivi ndivyo utakavyoitengeneza: Safina iwe na urefu wa dhiraa 300, upana wake dhiraa hamsini na kimo chake dhiraa thelathini.

  3. Itengenezee paa na umalizie safina kwa kuacha nafasi ya dhiraa moja juu. Weka mlango ubavuni mwa safina, na uifanye ya ghorofa ya chini, ya kati na ya juu.

  4. Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.

  5. Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.

  6. Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.

  7. Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.

  8. (Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)

  9. Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.

  10. Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.

  11. Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.

  12. Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”

  13. Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.

  14. Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,

  15. na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.

  16. Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,

  17. Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.

  18. Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,

  19. Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,

  20. Wahivi, Waariki, Wasini,

  21. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,

  22. na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.

  23. Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.

  24. Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.

  25. Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.