Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 12:22takriban 59 BK

    Lakini badala yake, vile viungo vya mwili vinavyoonekana kuwa dhaifu, ndivyo ambavyo ni vya muhimu sana.

  2. 1 Wakorintho 12:23takriban 59 BK

    Navyo vile viungo tunavyoviona havina heshima, ndivyo tunavipa heshima maalum. Vile viungo vya mwili ambavyo havina uzuri, tunavipa heshima ya pekee;

  3. 1 Wakorintho 12:24takriban 59 BK

    wakati vile viungo vyenye uzuri havihitaji utunzaji wa pekee. Lakini Mungu ameviweka pamoja viungo vya mwili na akavipa heshima zaidi vile vilivyopungukiwa,

  4. 1 Wakorintho 12:25takriban 59 BK

    ili pasiwe na mafarakano katika mwili, bali viungo vyote vihudumiane kwa usawa kila kimoja na mwenzake.

  5. 1 Wakorintho 12:26takriban 59 BK

    Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vyote huumia pamoja nacho, kama kiungo kimoja kikipewa heshima, viungo vyote hufurahi pamoja nacho.

  6. 1 Wakorintho 12:27takriban 59 BK

    Sasa ninyi ni mwili wa Kristo na kila mmoja wenu ni sehemu ya huo mwili.

  7. 1 Wakorintho 12:28takriban 59 BK

    Mungu ameweka katika kanisa, kwanza mitume, pili manabii, tatu walimu, kisha watenda miujiza, pia karama za kuponya, karama za kusaidiana, karama za uongozi, aina mbalimbali za lugha.

  8. 1 Wakorintho 12:29takriban 59 BK

    Je, wote ni mitume? Je, wote ni manabii? Je, wote ni walimu? Je, wote wanatenda miujiza?

  9. 1 Wakorintho 12:30takriban 59 BK

    Je, wote wana karama ya kuponya? Je, wote hunena kwa lugha mpya? Je, wote wanatafsiri?

  10. 1 Wakorintho 12:31takriban 59 BK

    Basi tamanini sana karama zilizo kuu. Nami nitawaonyesha njia iliyo bora zaidi.

  11. 1 Wakorintho 13:1takriban 59 BK

    Hata kama nitasema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa kengele inayolialia au toazi livumalo.

  12. 1 Wakorintho 13:2takriban 59 BK

    Ningekuwa na karama ya unabii na kujua siri zote na maarifa yote, hata kama nina imani kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu.

  13. 1 Wakorintho 13:3takriban 59 BK

    Kama nikitoa mali yote niliyo nayo na kama nikijitolea mwili wangu uchomwe moto, kama sina upendo, hainifaidi kitu.

  14. 1 Wakorintho 13:4takriban 59 BK

    Upendo huvumilia, upendo hufadhili, upendo hauoni wivu, hauna majivuno, hauna kiburi.

  15. 1 Wakorintho 13:5takriban 59 BK

    Haukosi kuwa na adabu, hautafuti mambo yake, haukasiriki upesi, hauweki kumbukumbu ya mabaya.

  16. 1 Wakorintho 13:6takriban 59 BK

    Upendo haufurahii mabaya bali hufurahi pamoja na kweli.

  17. 1 Wakorintho 13:7takriban 59 BK

    Upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.

  18. 1 Wakorintho 13:8takriban 59 BK

    Upendo haushindwi kamwe. Lakini ukiwepo unabii, utakoma; zikiwepo lugha, zitakoma; yakiwepo maarifa, yatapita.

  19. 1 Wakorintho 13:9takriban 59 BK

    Kwa maana tunafahamu kwa sehemu na tunatoa unabii kwa sehemu.

  20. 1 Wakorintho 13:10takriban 59 BK

    Lakini ukamilifu ukija, yale yasiyo kamili hutoweka.

  21. 1 Wakorintho 13:11takriban 59 BK

    Nilipokuwa mtoto, nilisema kama mtoto, niliwaza kama mtoto, nilifikiri kama mtoto. Nilipokuwa mtu mzima niliacha mambo ya kitoto.

  22. 1 Wakorintho 13:12takriban 59 BK

    Kwa maana sasa tunaona taswira kama kwa kioo, lakini wakati huo tutaona wazi. Sasa nafahamu kwa sehemu, wakati huo nitafahamu kikamilifu, kama vile mimi ninavyofahamika kikamilifu.

  23. 1 Wakorintho 13:13takriban 59 BK

    Basi sasa, yanadumu mambo haya matatu: Imani, tumaini na upendo. Lakini lililo kuu miongoni mwa haya matatu ni upendo.

  24. 1 Wakorintho 14:1takriban 59 BK

    Fuateni upendo na kutaka sana karama za roho, hasa karama ya unabii.

  25. 1 Wakorintho 14:2takriban 59 BK

    Kwa maana mtu yeyote anayesema kwa lugha, hasemi na wanadamu bali anasema na Mungu. Kwa kuwa hakuna mtu yeyote anayemwelewa, kwani anasema mambo ya siri kwa roho.