Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 11:6takriban 59 BK

    Kama mwanamke hatajifunika kichwa chake, basi inampasa kunyoa nywele zake. Lakini kama ni aibu kwa mwanamke kukata au kunyoa nywele zake, basi afunike kichwa chake.

  2. 1 Wakorintho 11:7takriban 59 BK

    Haimpasi mwanaume kufunika kichwa chake kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na utukufu wa Mungu, lakini mwanamke ni utukufu wa mwanaume.

  3. 1 Wakorintho 11:8takriban 59 BK

    Kwa maana mwanaume hakutoka kwa mwanamke, bali mwanamke alitoka kwa mwanaume.

  4. 1 Wakorintho 11:9takriban 59 BK

    Wala mwanaume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanaume.

  5. 1 Wakorintho 11:10takriban 59 BK

    Kwa sababu hii na kwa sababu ya malaika, inampasa mwanamke awe na ishara ya mamlaka juu yake.

  6. 1 Wakorintho 11:11takriban 59 BK

    Lakini katika Bwana, mwanamke hajitegemei pasipo mwanaume na mwanaume hajitegemei pasipo mwanamke.

  7. 1 Wakorintho 11:12takriban 59 BK

    Kama vile mwanamke alivyoumbwa kutoka kwa mwanaume, vivyo hivyo mwanaume huzaliwa na mwanamke. Lakini vitu vyote vyatoka kwa Mungu.

  8. 1 Wakorintho 11:13takriban 59 BK

    Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa kwa mwanamke kumwomba Mungu bila kufunika kichwa chake?

  9. 1 Wakorintho 11:14takriban 59 BK

    Je, maumbile ya asili hayatufundishi kuwa ni aibu kwa mwanaume kuwa na nywele ndefu?

  10. 1 Wakorintho 11:15takriban 59 BK

    Lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu ni utukufu kwake? Kwa maana mwanamke amepewa nywele ndefu ili kumfunika.

  11. 1 Wakorintho 11:16takriban 59 BK

    Kama mtu anataka kubishana juu ya jambo hili, sisi wala makanisa ya Mungu hatutambui desturi nyingine.

  12. 1 Wakorintho 11:17takriban 59 BK

    Basi katika maagizo yafuatayo, siwezi kuwasifu, kwa sababu mkutanikapo si kwa ajili ya faida bali kwa hasara.

  13. 1 Wakorintho 11:18takriban 59 BK

    Kwanza, mnapokutana kama kanisa, nasikia kwamba kuna mgawanyiko miongoni mwenu, nami kwa kiasi fulani nasadiki kuwa ndivyo ilivyo.

  14. 1 Wakorintho 11:19takriban 59 BK

    Bila shaka lazima pawe na tofauti miongoni mwenu ili kuonyesha ni nani anayekubaliwa na Mungu.

  15. 1 Wakorintho 11:20takriban 59 BK

    Mkutanikapo pamoja si chakula cha Bwana mnachokula,

  16. 1 Wakorintho 11:21takriban 59 BK

    kwa kuwa mnapokula, kila mmoja wenu anakula bila kuwangoja wengine. Mmoja hukaa njaa na mwingine analewa.

  17. 1 Wakorintho 11:22takriban 59 BK

    Je, hamna nyumbani kwenu ambako mnaweza kula na kunywa? Au mnalidharau kanisa la Mungu na kuwadhalilisha wale wasio na kitu? Niwaambie nini? Je, niwasifu juu ya jambo hili? La, hasha!

  18. 1 Wakorintho 11:23takriban 59 BK

    Kwa maana mimi nilipokea kutoka kwa Bwana yale niliyowapa ninyi, kwamba Bwana Yesu, usiku ule aliposalitiwa, alitwaa mkate,

  19. 1 Wakorintho 11:24takriban 59 BK

    naye akiisha kushukuru, akaumega, akasema, “Huu ndio mwili wangu, uliotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.”

  20. 1 Wakorintho 11:25takriban 59 BK

    Vivyo hivyo baada ya kula, akakitwaa kikombe, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu. Fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu.”

  21. 1 Wakorintho 11:26takriban 59 BK

    Maana kila mlapo mkate huu na kunywea kikombe hiki, mnatangaza mauti ya Bwana mpaka ajapo.

  22. 1 Wakorintho 11:27takriban 59 BK

    Kwa hiyo, mtu yeyote alaye mkate huo au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa na hatia ya dhambi juu ya mwili na damu ya Bwana.

  23. 1 Wakorintho 11:28takriban 59 BK

    Inampasa mtu ajichunguze mwenyewe, kabla ya kula mkate na kukinywea kikombe.

  24. 1 Wakorintho 11:29takriban 59 BK

    Kwa maana mtu yeyote alaye na kunywa pasipo kuutambua mwili wa Bwana, hula na kunywa hukumu juu yake mwenyewe.

  25. 1 Wakorintho 11:30takriban 59 BK

    Hii ndiyo sababu wengi miongoni mwenu ni wagonjwa na dhaifu na wengine wenu hata wamekufa.