Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 9:16takriban 59 BK

    Lakini ninapohubiri Injili siwezi kujisifu maana ninalazimika kuhubiri. Ole wangu nisipoihubiri Injili!

  2. 1 Wakorintho 9:17takriban 59 BK

    Nikihubiri kwa hiari, ninayo thawabu. Lakini kama si kwa hiari, basi ninachofanya ni kutekeleza tu uwakili niliowekewa.

  3. 1 Wakorintho 9:18takriban 59 BK

    Basi je, thawabu yangu ni nini? Thawabu yangu ni hii: Ya kwamba katika kuhubiri Injili niitoe bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.

  4. 1 Wakorintho 9:19takriban 59 BK

    Ingawa mimi ni huru, wala si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya kuwa mtumwa wa kila mtu, ili niweze kuwavuta wengi kadri iwezekanavyo.

  5. 1 Wakorintho 9:20takriban 59 BK

    Kwa Wayahudi, nilikuwa kama Myahudi, ili niwapate Wayahudi. Kwa watu wale walio chini ya sheria, nilikuwa kama aliye chini ya sheria (ingawa mimi siko chini ya sheria), ili niweze kuwapata wale walio chini ya sheria.

  6. 1 Wakorintho 9:21takriban 59 BK

    Kwa watu wasio na sheria nilikuwa kama asiye na sheria (ingawa siko huru mbali na sheria ya Mungu, bali niko chini ya sheria ya Kristo), ili niweze kuwapata wale wasio na sheria.

  7. 1 Wakorintho 9:22takriban 59 BK

    Kwa walio dhaifu nilikuwa dhaifu, ili niweze kuwapata walio dhaifu. Nimekuwa mtu wa hali zote kwa watu wote ili kwa njia yoyote niweze kuwaokoa baadhi yao.

  8. 1 Wakorintho 9:23takriban 59 BK

    Nafanya haya yote kwa ajili ya Injili, ili nipate kushiriki baraka zake.

  9. 1 Wakorintho 9:24takriban 59 BK

    Je, hamjui kwamba katika mashindano ya mbio wote wanaoshindana hukimbia, lakini ni mmoja wao tu apewaye tuzo? Kwa hiyo kimbieni katika mashindano kwa jinsi ambavyo mtapata tuzo.

  10. 1 Wakorintho 9:25takriban 59 BK

    Kila mmoja anayeshiriki katika mashindano hufanya mazoezi makali. Wao hufanya hivyo ili wapokee taji isiyodumu, lakini sisi tunafanya hivyo ili kupata taji idumuyo milele.

  11. 1 Wakorintho 9:26takriban 59 BK

    Kwa hiyo mimi sikimbii kama mtu akimbiaye bila lengo, sipigani kama mtu anayepiga hewa,

  12. 1 Wakorintho 9:27takriban 59 BK

    la, bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha ili nikiisha kuwahubiria wengine, mimi nisiwe mtu wa kukataliwa.

  13. 1 Wakorintho 10:1takriban 59 BK

    Ndugu zangu, sitaki mkose kufahamu ukweli huu kwamba baba zetu walikuwa wote chini ya wingu na kwamba wote walipita katikati ya bahari.

  14. 1 Wakorintho 10:2takriban 59 BK

    Wote wakabatizwa kuwa wa Mose ndani ya lile wingu na ndani ya ile bahari.

  15. 1 Wakorintho 10:3takriban 59 BK

    Wote walikula chakula kile kile cha roho,

  16. 1 Wakorintho 10:4takriban 59 BK

    na wote wakanywa kile kile kinywaji cha roho, kwa maana walikunywa kutoka ule mwamba wa roho uliofuatana nao, nao ule mwamba ulikuwa Kristo.

  17. 1 Wakorintho 10:5takriban 59 BK

    Lakini Mungu hakupendezwa na wengi wao, kwa hiyo miili yao ilitapakaa jangwani.

  18. 1 Wakorintho 10:6takriban 59 BK

    Basi mambo haya yalitokea kama mifano ili kutuzuia tusiweke mioyo yetu katika mambo maovu kama wao walivyofanya.

  19. 1 Wakorintho 10:7takriban 59 BK

    Msiwe waabudu sanamu, kama baadhi yao walivyokuwa, kama ilivyoandikwa, “Watu waliketi chini kula na kunywa, kisha wakainuka kucheza na kufanya sherehe za kipagani.”

  20. 1 Wakorintho 10:8takriban 59 BK

    Wala tusifanye uzinzi kama baadhi yao walivyofanya, wakafa watu 23,000 kwa siku moja.

  21. 1 Wakorintho 10:9takriban 59 BK

    Wala tusimjaribu Kristo, kama baadhi yao walivyofanya, wakafa kwa kuumwa na nyoka.

  22. 1 Wakorintho 10:10takriban 59 BK

    Msinungʼunike kama baadhi yao walivyofanya, wakaangamizwa na mharabu.

  23. 1 Wakorintho 10:11takriban 59 BK

    Mambo haya yote yaliwapata wao ili yawe mifano kwa wengine, nayo yaliandikwa ili yatuonye sisi ambao mwisho wa nyakati umetufikia.

  24. 1 Wakorintho 10:12takriban 59 BK

    Hivyo, yeye ajidhaniaye amesimama, aangalie asianguke.

  25. 1 Wakorintho 10:13takriban 59 BK

    Hakuna jaribu lolote lililowapata ambalo si la kawaida kwa wanadamu. Naye Mungu ni mwaminifu; hataruhusu mjaribiwe kupita mnavyoweza. Lakini mnapojaribiwa atawapa njia ya kutokea ili mweze kustahimili.