Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 10:14takriban 59 BK

    Kwa hiyo wapenzi wangu, zikimbieni ibada za sanamu.

  2. 1 Wakorintho 10:15takriban 59 BK

    Nasema watu wenye ufahamu, amueni wenyewe kuhusu haya niyasemayo.

  3. 1 Wakorintho 10:16takriban 59 BK

    Je, kikombe cha baraka ambacho tunakibariki, si ushirika katika damu ya Kristo? Mkate tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?

  4. 1 Wakorintho 10:17takriban 59 BK

    Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja, kwa kuwa wote twashiriki mkate mmoja.

  5. 1 Wakorintho 10:18takriban 59 BK

    Waangalieni watu wa Israeli: Je, wale wote walao dhabihu si ni wale watendao kazi madhabahuni?

  6. 1 Wakorintho 10:19takriban 59 BK

    Je, nina maana kwamba kafara iliyotolewa kwa sanamu ni kitu chenye maana yoyote? Au kwamba sanamu ni kitu chenye maana yoyote?

  7. 1 Wakorintho 10:20takriban 59 BK

    La hasha! Lakini kafara za watu wasiomjua Mungu hutolewa kwa mashetani, wala si kwa Mungu. Nami sitaki ninyi mwe na ushirika na mashetani.

  8. 1 Wakorintho 10:21takriban 59 BK

    Hamwezi kunywa katika kikombe cha Bwana na cha mashetani pia. Hamwezi kuwa na sehemu katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani pia.

  9. 1 Wakorintho 10:22takriban 59 BK

    Je, tunataka kuamsha wivu wa Bwana? Je, sisi tuna nguvu kuliko yeye?

  10. 1 Wakorintho 10:23takriban 59 BK

    “Vitu vyote ni halali,” lakini si vitu vyote vilivyo na faida. “Vitu vyote ni halali,” lakini si vyote vinavyojenga.

  11. 1 Wakorintho 10:24takriban 59 BK

    Mtu yeyote asitafute yaliyo yake mwenyewe, bali kila mtu atafute yale yanayowafaa wengine.

  12. 1 Wakorintho 10:25takriban 59 BK

    Kuleni chochote kinachouzwa sokoni, bila kuuliza swali lolote kwa ajili ya dhamiri.

  13. 1 Wakorintho 10:26takriban 59 BK

    Kwa maana, “Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana.”

  14. 1 Wakorintho 10:27takriban 59 BK

    Kama ukikaribishwa chakula na mtu asiyeamini nawe ukikubali kwenda, kula kila kitu kitakachowekwa mbele yako bila kuuliza maswali kwa ajili ya dhamiri.

  15. 1 Wakorintho 10:28takriban 59 BK

    Lakini kama mtu yeyote akikuambia, “Hiki kimetolewa kafara kwa sanamu,” basi usikile kwa ajili ya huyo aliyekuambia na kwa ajili ya dhamiri.

  16. 1 Wakorintho 10:29takriban 59 BK

    Nina maana dhamiri ya huyo aliyekuambia, wala si kwa ajili ya dhamiri yako. Lakini kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?

  17. 1 Wakorintho 10:30takriban 59 BK

    Kama nikila kwa shukrani, kwa nini nashutumiwa kwa kile ambacho kwa hicho ninamshukuru Mungu?

  18. 1 Wakorintho 10:31takriban 59 BK

    Basi, lolote mfanyalo, kama ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.

  19. 1 Wakorintho 10:32takriban 59 BK

    Msiwe kikwazo kwa mtu yeyote, wawe Wayahudi au Wayunani, au kwa kanisa la Mungu,

  20. 1 Wakorintho 10:33takriban 59 BK

    kama hata mimi ninavyojaribu kumpendeza kila mtu kwa kila namna. Kwa maana sitafuti mema kwa ajili yangu mwenyewe bali kwa ajili ya wengi, ili waweze kuokolewa.

  21. 1 Wakorintho 11:1takriban 59 BK

    Igeni mfano wangu, kama ninavyouiga mfano wa Kristo.

  22. 1 Wakorintho 11:2takriban 59 BK

    Ninawasifu kwa kuwa mnanikumbuka katika kila jambo na kwa kushika mafundisho niliyowapa.

  23. 1 Wakorintho 11:3takriban 59 BK

    Napenda mfahamu kwamba kichwa cha kila mwanaume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanaume, nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.

  24. 1 Wakorintho 11:4takriban 59 BK

    Kila mwanaume anayeomba au kutoa unabii akiwa amefunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake.

  25. 1 Wakorintho 11:5takriban 59 BK

    Naye kila mwanamke anayeomba au kutoa unabii pasipo kufunika kichwa chake, anakiaibisha kichwa chake, kwani ni sawa na yeye aliyenyoa nywele.