Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 14:3takriban 59 BK

    Lakini anayetoa unabii anasema na watu akiwajenga, kuwatia moyo na kuwafariji.

  2. 1 Wakorintho 14:4takriban 59 BK

    Anenaye kwa lugha hujijenga mwenyewe, bali atoaye unabii hulijenga kanisa.

  3. 1 Wakorintho 14:5takriban 59 BK

    Ningependa kila mmoja wenu anene kwa lugha lakini ningependa zaidi nyote mtoe unabii. Kwa kuwa yeye atoaye unabii ni mkuu kuliko anenaye kwa lugha, isipokuwa atafsiri, ili kanisa lipate kujengwa.

  4. 1 Wakorintho 14:6takriban 59 BK

    Sasa ndugu zangu, kama nikija kwenu nikasema kwa lugha mpya nitawafaidia nini kama sikuwaletea ufunuo au neno la maarifa au unabii au mafundisho?

  5. 1 Wakorintho 14:7takriban 59 BK

    Hata vitu visivyo na uhai vitoapo sauti, kama vile filimbi au kinubi, mtu atajuaje ni wimbo gani unaoimbwa kusipokuwa na tofauti ya upigaji?

  6. 1 Wakorintho 14:8takriban 59 BK

    Tena kama tarumbeta haitoi sauti inayoeleweka, ni nani atakayejiandaa kwa ajili ya vita?

  7. 1 Wakorintho 14:9takriban 59 BK

    Vivyo hivyo na ninyi, kama mkinena maneno yasiyoeleweka katika akili, mtu atajuaje mnalosema? Kwa maana mtakuwa mnasema hewani tu.

  8. 1 Wakorintho 14:10takriban 59 BK

    Bila shaka ziko sauti nyingi ulimwenguni, wala hakuna isiyo na maana.

  9. 1 Wakorintho 14:11takriban 59 BK

    Basi kama sielewi maana ya hiyo sauti, nitakuwa mgeni kwa yule msemaji, naye atakuwa mgeni kwangu.

  10. 1 Wakorintho 14:12takriban 59 BK

    Vivyo hivyo na ninyi. Kwa kuwa mnatamani kuwa na karama za rohoni, jitahidini kuzidi sana katika karama kwa ajili ya kulijenga kanisa.

  11. 1 Wakorintho 14:13takriban 59 BK

    Kwa sababu hii, yeye anenaye kwa lugha na aombe kwamba apate kutafsiri kile anachonena.

  12. 1 Wakorintho 14:14takriban 59 BK

    Kwa maana nikiomba kwa lugha, roho yangu inaomba, lakini akili yangu haina matunda.

  13. 1 Wakorintho 14:15takriban 59 BK

    Nifanyeje basi? Nitaomba kwa roho, na pia nitaomba kwa akili yangu. Nitaimba kwa roho na nitaimba kwa akili yangu pia.

  14. 1 Wakorintho 14:16takriban 59 BK

    Ikiwa unabariki kwa roho, mtu mwingine atakayejikuta miongoni mwa hao wasiojua, atawezaje kusema “Amen” katika kushukuru kwako, wakati haelewi unachosema?

  15. 1 Wakorintho 14:17takriban 59 BK

    Mnaweza kuwa mnatoa shukrani kweli, sawa, lakini huyo mtu mwingine hajengeki.

  16. 1 Wakorintho 14:18takriban 59 BK

    Namshukuru Mungu kwamba mimi nanena kwa lugha kuliko ninyi nyote.

  17. 1 Wakorintho 14:19takriban 59 BK

    Lakini ndani ya kanisa ni afadhali niseme maneno matano ya kueleweka ili niwafundishe wengine kuliko kusema maneno 10,000 kwa lugha.

  18. 1 Wakorintho 14:20takriban 59 BK

    Ndugu zangu, msiwe kama watoto katika kufikiri kwenu, afadhali kuhusu uovu mwe kama watoto wachanga, lakini katika kufikiri kwenu, mwe watu wazima.

  19. 1 Wakorintho 14:21takriban 59 BK

    Katika Sheria imeandikwa kwamba: “Kupitia kwa watu wenye lugha ngʼeni na kupitia midomo ya wageni, nitasema na watu hawa, lakini hata hivyo hawatanisikiliza,” asema Bwana.

  20. 1 Wakorintho 14:22takriban 59 BK

    Basi kunena kwa lugha ni ishara, si kwa watu waaminio, bali kwa wasioamini, wakati unabii si kwa ajili ya wasioamini, bali kwa ajili ya waaminio.

  21. 1 Wakorintho 14:23takriban 59 BK

    Kwa hiyo kama kanisa lote likikutana na kila mmoja akanena kwa lugha, kisha wakaingia wageni wasioelewa wasioamini, je, hawatasema kwamba wote mna wazimu?

  22. 1 Wakorintho 14:24takriban 59 BK

    Lakini kama mtu asiyeamini au asiyeelewa akiingia wakati kila mtu anatoa unabii, ataaminishwa na watu wote kuwa yeye ni mwenye dhambi na kuhukumiwa na wote,

  23. 1 Wakorintho 14:25takriban 59 BK

    nazo siri za moyo wake zitawekwa wazi. Kwa hiyo ataanguka chini na kumwabudu Mungu akikiri, “Kweli Mungu yuko katikati yenu!”

  24. 1 Wakorintho 14:26takriban 59 BK

    Basi tuseme nini ndugu zangu? Mnapokutana pamoja, kila mmoja ana wimbo, au neno la mafundisho, au ufunuo, lugha mpya au atatafsiri. Mambo yote yatendeke kwa ajili ya kulijenga kanisa.

  25. 1 Wakorintho 14:27takriban 59 BK

    Kama mtu yeyote akinena kwa lugha, basi waseme watu wawili au watatu si zaidi, mmoja baada ya mwingine na lazima awepo mtu wa kutafsiri.