Rukia maudhui

circa 605–538 BC

The Babylonian Exile

Jerusalem falls and the temple burns; Ezekiel and Daniel minister among the exiles as Lamentations mourns the city's ruin.

1,784 mistari · 3 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Maombolezo 4:16takriban 588 KK

    Bwana mwenyewe amewatawanya; hawaangalii tena. Makuhani hawaonyeshwi heshima, wazee hawakubaliki.

  2. Maombolezo 4:17takriban 588 KK

    Zaidi ya hayo, macho yetu yalichoka, kwa kutazamia bure msaada; tuliangalia kutoka minara yetu kwa taifa lisiloweza kutuokoa.

  3. Maombolezo 4:18takriban 588 KK

    Watu walituvizia katika kila hatua hata hatukuweza kutembea katika barabara zetu. Mwisho wetu ulikuwa karibu, siku zetu zilikuwa zimetimia, kwa maana mwisho wetu ulikuwa umefika.

  4. Maombolezo 4:19takriban 588 KK

    Waliotufuatia walikuwa wepesi kuliko tai angani; walitusaka juu milimani na kutuvizia jangwani.

  5. Maombolezo 4:20takriban 588 KK

    Mpakwa mafuta wa Bwana, pumzi ya uhai wetu hasa, alinaswa katika mitego yao. Tulifikiri kwamba chini ya kivuli chake tungeliweza kuishi miongoni mwa mataifa.

  6. Maombolezo 4:21takriban 588 KK

    Shangilia na ufurahi, ee Binti Edomu, wewe unayeishi nchi ya Usi. Lakini kwako pia kikombe kitapitishwa, Utalewa na kuvuliwa nguo ubaki uchi.

  7. Maombolezo 4:22takriban 588 KK

    Ee Binti Sayuni, adhabu yako itaisha, hatarefusha muda wako wa kukaa uhamishoni. Lakini, ee Binti Edomu, ataadhibu dhambi yako, na atafunua uovu wako.

  8. Maombolezo 5:1takriban 588 KK

    Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.

  9. Maombolezo 5:2takriban 588 KK

    Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.

  10. Maombolezo 5:3takriban 588 KK

    Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.

  11. Maombolezo 5:4takriban 588 KK

    Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.

  12. Maombolezo 5:5takriban 588 KK

    Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.

  13. Maombolezo 5:6takriban 588 KK

    Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.

  14. Maombolezo 5:7takriban 588 KK

    Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.

  15. Maombolezo 5:8takriban 588 KK

    Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.

  16. Maombolezo 5:9takriban 588 KK

    Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.

  17. Maombolezo 5:10takriban 588 KK

    Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.

  18. Maombolezo 5:11takriban 588 KK

    Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.

  19. Maombolezo 5:12takriban 588 KK

    Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.

  20. Maombolezo 5:13takriban 588 KK

    Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.

  21. Maombolezo 5:14takriban 588 KK

    Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.

  22. Maombolezo 5:15takriban 588 KK

    Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.

  23. Maombolezo 5:16takriban 588 KK

    Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!

  24. Maombolezo 5:17takriban 588 KK

    Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,

  25. Maombolezo 5:18takriban 588 KK

    kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.