- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 605–538 BC
The Babylonian Exile
Jerusalem falls and the temple burns; Ezekiel and Daniel minister among the exiles as Lamentations mourns the city's ruin.
Mistari ya kipindi hiki
- Maombolezo 3:57takriban 588 KK
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
- Maombolezo 3:58takriban 588 KK
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
- Maombolezo 3:59takriban 588 KK
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
- Maombolezo 3:60takriban 588 KK
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
- Maombolezo 3:61takriban 588 KK
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
- Maombolezo 3:62takriban 588 KK
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
- Maombolezo 3:63takriban 588 KK
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
- Maombolezo 3:64takriban 588 KK
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
- Maombolezo 3:65takriban 588 KK
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
- Maombolezo 3:66takriban 588 KK
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.
- Maombolezo 4:1takriban 588 KK
Jinsi dhahabu ilivyopoteza mngʼao wake, dhahabu iliyo safi haingʼai! Vito vya thamani vimetawanywa kwenye mwanzo wa kila barabara.
- Maombolezo 4:2takriban 588 KK
Wana wa Sayuni wenye thamani, ambao mwanzo uzito wa thamani yao ulikuwa wa dhahabu, sasa wanaangaliwa kama vyungu vya udongo, kazi ya mikono ya mfinyanzi!
- Maombolezo 4:3takriban 588 KK
Hata mbweha hutoa matiti yao kunyonyesha watoto wao, lakini watu wangu wamekuwa wasio na huruma kama mbuni jangwani.
- Maombolezo 4:4takriban 588 KK
Kwa sababu ya kiu ulimi wa mtoto mchanga umegandamana na kaakaa la kinywa chake, watoto huomba mkate, lakini hakuna yeyote awapaye.
- Maombolezo 4:5takriban 588 KK
Wale waliokula vyakula vya kifahari ni maskini barabarani. Wale waliokuzwa wakivaa nguo za zambarau sasa wanalalia majivu.
- Maombolezo 4:6takriban 588 KK
Adhabu ya watu wangu ni kubwa kuliko ile ya Sodoma, ambayo ilipinduliwa ghafula bila kuwepo mkono wa msaada.
- Maombolezo 4:7takriban 588 KK
Wakuu wao walikuwa wamengʼaa kuliko theluji na weupe kuliko maziwa, miili yao ilikuwa myekundu kuliko marijani, kuonekana kwao kama yakuti samawi.
- Maombolezo 4:8takriban 588 KK
Lakini sasa ni weusi kuliko masizi; hawatambulikani barabarani. Ngozi yao imeshikamana juu ya mifupa yao, imekuwa mikavu kama fimbo.
- Maombolezo 4:9takriban 588 KK
Wale waliouawa kwa upanga ni bora kuliko wale wanaokufa njaa; wanateseka kwa njaa, wanatokomea kwa kukosa chakula kutoka shambani.
- Maombolezo 4:10takriban 588 KK
Kwa mikono yao wenyewe wanawake wenye huruma wanapika watoto wao wenyewe, waliokuwa chakula chao watu wangu walipoangamizwa.
- Maombolezo 4:11takriban 588 KK
Bwana ametoa nafasi kamilifu ya ghadhabu yake; ameimwaga hasira yake kali. Amewasha moto katika Sayuni ambao umeteketeza misingi yake.
- Maombolezo 4:12takriban 588 KK
Wafalme wa dunia hawakuamini, wala mtu yeyote wa duniani, kwamba adui na watesi wangeweza kuingia kwenye malango ya Yerusalemu.
- Maombolezo 4:13takriban 588 KK
Lakini hili lilitokea kwa sababu ya dhambi za manabii wake, na maovu ya makuhani wake, waliomwaga ndani yake damu ya wenye haki.
- Maombolezo 4:14takriban 588 KK
Sasa wanapapasa papasa barabarani kama watu ambao ni vipofu. Wamenajisiwa kabisa kwa damu, hata hakuna anayethubutu kugusa mavazi yao.
- Maombolezo 4:15takriban 588 KK
Watu wanawapigia kelele, “Ondokeni! Ninyi ni najisi! Ondokeni! Ondokeni! Msituguse!” Wanapokimbia na kutangatanga huku na huko, watu miongoni mwa mataifa wanasema, “Hawawezi kukaa hapa zaidi.”