- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 605–538 BC
The Babylonian Exile
Jerusalem falls and the temple burns; Ezekiel and Daniel minister among the exiles as Lamentations mourns the city's ruin.
Mistari ya kipindi hiki
- Maombolezo 3:7takriban 588 KK
Amenizungushia ukuta ili nisiweze kutoroka, amenifunga kwa minyororo mizito.
- Maombolezo 3:8takriban 588 KK
Hata ninapoita au kulia ili kuomba msaada, anakataa kupokea maombi yangu.
- Maombolezo 3:9takriban 588 KK
Ameizuia njia yangu kwa mapande ya mawe, amepotosha njia zangu.
- Maombolezo 3:10takriban 588 KK
Kama dubu aviziaye, kama simba mafichoni,
- Maombolezo 3:11takriban 588 KK
ameniburuta kutoka njia, akanirarua na kuniacha bila msaada.
- Maombolezo 3:12takriban 588 KK
Amevuta upinde wake na kunifanya mimi niwe lengo kwa ajili ya mishale yake.
- Maombolezo 3:13takriban 588 KK
Alinichoma moyo wangu kwa mishale iliyotoka kwenye podo lake.
- Maombolezo 3:14takriban 588 KK
Nimekuwa kichekesho kwa watu wangu wote, wananidhihaki kwa wimbo mchana kutwa.
- Maombolezo 3:15takriban 588 KK
Amenijaza kwa majani machungu na kunishibisha kwa nyongo.
- Maombolezo 3:16takriban 588 KK
Amevunja meno yangu kwa changarawe, amenikanyagia mavumbini.
- Maombolezo 3:17takriban 588 KK
Amani yangu imeondolewa, nimesahau kufanikiwa ni nini.
- Maombolezo 3:18takriban 588 KK
Kwa hiyo nasema, “Fahari yangu imeondoka na yale yote niliyokuwa nimetarajia kutoka kwa Bwana.”
- Maombolezo 3:19takriban 588 KK
Nayakumbuka mateso yangu na kutangatanga kwangu, uchungu na nyongo.
- Maombolezo 3:20takriban 588 KK
Ninayakumbuka vyema, nayo nafsi yangu imezimia ndani yangu.
- Maombolezo 3:21takriban 588 KK
Hata hivyo najikumbusha neno hili na kwa hiyo ninalo tumaini.
- Maombolezo 3:22takriban 588 KK
Kwa sababu ya upendo mkuu wa Bwana, hatuangamii, kwa kuwa huruma zake hazikomi kamwe.
- Maombolezo 3:23takriban 588 KK
Ni mpya kila asubuhi, uaminifu wako ni mkuu.
- Maombolezo 3:24takriban 588 KK
Nimeiambia nafsi yangu, “Bwana ni fungu langu, kwa hiyo nitamngojea.”
- Maombolezo 3:25takriban 588 KK
Bwana ni mwema kwa wale ambao tumaini lao ni kwake, kwa yule ambaye humtafuta;
- Maombolezo 3:26takriban 588 KK
ni vyema kungojea kwa utulivu kwa ajili ya wokovu wa Bwana.
- Maombolezo 3:27takriban 588 KK
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
- Maombolezo 3:28takriban 588 KK
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
- Maombolezo 3:29takriban 588 KK
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
- Maombolezo 3:30takriban 588 KK
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
- Maombolezo 3:31takriban 588 KK
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.