- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 605–538 BC
The Babylonian Exile
Jerusalem falls and the temple burns; Ezekiel and Daniel minister among the exiles as Lamentations mourns the city's ruin.
Mistari ya kipindi hiki
- Maombolezo 3:32takriban 588 KK
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
- Maombolezo 3:33takriban 588 KK
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
- Maombolezo 3:34takriban 588 KK
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
- Maombolezo 3:35takriban 588 KK
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
- Maombolezo 3:36takriban 588 KK
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
- Maombolezo 3:37takriban 588 KK
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
- Maombolezo 3:38takriban 588 KK
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
- Maombolezo 3:39takriban 588 KK
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
- Maombolezo 3:40takriban 588 KK
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
- Maombolezo 3:41takriban 588 KK
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
- Maombolezo 3:42takriban 588 KK
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
- Maombolezo 3:43takriban 588 KK
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
- Maombolezo 3:44takriban 588 KK
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
- Maombolezo 3:45takriban 588 KK
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
- Maombolezo 3:46takriban 588 KK
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
- Maombolezo 3:47takriban 588 KK
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
- Maombolezo 3:48takriban 588 KK
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
- Maombolezo 3:49takriban 588 KK
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
- Maombolezo 3:50takriban 588 KK
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
- Maombolezo 3:51takriban 588 KK
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
- Maombolezo 3:52takriban 588 KK
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
- Maombolezo 3:53takriban 588 KK
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
- Maombolezo 3:54takriban 588 KK
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
- Maombolezo 3:55takriban 588 KK
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
- Maombolezo 3:56takriban 588 KK
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”