- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Sin
Mistari muhimu ya Biblia
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.
Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.
Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.
Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;
tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.
Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.
Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
Wapumbavu hudhihaki kujirekebisha kutoka dhambi, bali wema hupatikana miongoni mwa wanyofu.
Haki huinua taifa, bali dhambi ni aibu kwa watu wote.
Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.
Kwa upendo na uaminifu uovu huondolewa; kwa kumcha Bwana mtu hujiepusha na ubaya.
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
wale ambao ni safi machoni pao wenyewe kumbe hawakuoshwa uchafu wao;