Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Mathayo 1:1takriban 26 BK

    Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Abrahamu:

  2. Mathayo 1:2takriban 26 BK

    Abrahamu akamzaa Isaki, Isaki akamzaa Yakobo, Yakobo akawazaa Yuda na ndugu zake,

  3. Mathayo 1:3takriban 26 BK

    Yuda akawazaa Peresi na Zera, ambao mama yao alikuwa Tamari, Peresi akamzaa Hesroni, Hesroni akamzaa Aramu,

  4. Mathayo 1:4takriban 26 BK

    Aramu akamzaa Aminadabu, Aminadabu akamzaa Nashoni, Nashoni akamzaa Salmoni,

  5. Mathayo 1:5takriban 26 BK

    Salmoni akamzaa Boazi, na mama yake Boazi alikuwa Rahabu, Boazi akamzaa Obedi, ambaye mama yake alikuwa Ruthu, Obedi akamzaa Yese,

  6. Mathayo 1:6takriban 26 BK

    Yese akamzaa Daudi ambaye alikuwa mfalme. Daudi akamzaa Solomoni, ambaye mama yake ni yule aliyekuwa mke wa Uria.

  7. Mathayo 1:7takriban 26 BK

    Solomoni akamzaa Rehoboamu, Rehoboamu akamzaa Abiya, Abiya akamzaa Asa,

  8. Mathayo 1:8takriban 26 BK

    Asa akamzaa Yehoshafati, Yehoshafati akamzaa Yoramu, Yoramu akamzaa Uzia,

  9. Mathayo 1:9takriban 26 BK

    Uzia akamzaa Yothamu, Yothamu akamzaa Ahazi, Ahazi akamzaa Hezekia,

  10. Mathayo 1:10takriban 26 BK

    Hezekia akamzaa Manase, Manase akamzaa Amoni, Amoni akamzaa Yosia,

  11. Mathayo 1:11takriban 26 BK

    wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake.

  12. Mathayo 1:12takriban 26 BK

    Baada ya uhamisho wa Babeli: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli akamzaa Zerubabeli,

  13. Mathayo 1:13takriban 26 BK

    Zerubabeli akamzaa Abiudi, Abiudi akamzaa Eliakimu, Eliakimu akamzaa Azori,

  14. Mathayo 1:14takriban 26 BK

    Azori akamzaa Sadoki, Sadoki akamzaa Akimu, Akimu akamzaa Eliudi,

  15. Mathayo 1:15takriban 26 BK

    Eliudi akamzaa Eleazari, Eleazari akamzaa Matani, Matani akamzaa Yakobo,

  16. Mathayo 1:16takriban 26 BK

    naye Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa mumewe Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.

  17. Mathayo 1:17takriban 26 BK

    Hivyo, kulikuwepo na jumla ya vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli, na vizazi kumi na vinne tangu wakati wa uhamisho kwenda utumwani Babeli hadi Kristo.

  18. Mathayo 1:18takriban 26 BK

    Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria alionekana kuwa na mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

  19. Mathayo 1:19takriban 26 BK

    Kwa kuwa Yosefu, mwanaume aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani, aliazimu kumwacha kwa siri.

  20. Mathayo 1:20takriban 26 BK

    Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili, malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na kusema, “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

  21. Mathayo 1:21takriban 26 BK

    Naye atamzaa mwana, nawe utamwita Jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye atakayewaokoa watu wake kutoka dhambi zao.”

  22. Mathayo 1:22takriban 26 BK

    Haya yote yalitukia ili litimie lile Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii, akisema:

  23. Mathayo 1:23takriban 26 BK

    “Tazama, bikira atachukua mimba, naye atamzaa mwana, nao watamwita Jina lake Imanueli”: maana yake, “Mungu pamoja nasi.”

  24. Mathayo 1:24takriban 26 BK

    Yosefu alipoamka kutoka usingizini, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake.

  25. Mathayo 1:25takriban 26 BK

    Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria alipojifungua mwanawe kifungua mimba akamwita Jina lake Yesu.