Rukia maudhui

circa 6 BC – AD 30

The Life of Jesus

The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.

3,779 mistari · 4 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

  2. Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.

  3. Yohana 1:3takriban 4004 KK

    Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.

  4. Yohana 1:4takriban 4004 KK

    Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.

  5. Yohana 1:5takriban 4004 KK

    Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.

  6. Yohana 1:6takriban 5 BK

    Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.

  7. Yohana 1:7takriban 5 BK

    Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.

  8. Yohana 1:8takriban 5 BK

    Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.

  9. Yohana 1:9takriban 5 BK

    Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.

  10. Yohana 1:10takriban 5 BK

    Huyo Neno alikuwako ulimwenguni na ingawa ulimwengu uliumbwa kupitia kwake, haukumtambua.

  11. Yohana 1:11takriban 5 BK

    Alikuja kwa walio wake, lakini wao hawakumpokea.

  12. Yohana 1:12takriban 5 BK

    Bali wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake.

  13. Yohana 1:13takriban 5 BK

    Hawa ndio wasiozaliwa kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili au kwa mapenzi ya mtu, bali kwa mapenzi ya Mungu.

  14. Yohana 1:14takriban 5 BK

    Neno alifanyika mwili, akakaa miongoni mwetu, nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba, amejaa neema na kweli.

  15. Yohana 1:15takriban 5 BK

    Yohana alishuhudia habari zake, akapaza sauti, akisema, “Huyu ndiye yule niliyewaambia kwamba, ‘Yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuniliko mimi, kwa kuwa alikuwepo kabla yangu.’ ”

  16. Yohana 1:16takriban 5 BK

    Kutokana na ukamilifu wake, sisi sote tumepokea neema juu ya neema.

  17. Yohana 1:17takriban 5 BK

    Kwa kuwa sheria ilitolewa kwa mkono wa Mose, lakini neema na kweli imekuja kupitia Yesu Kristo.

  18. Yohana 1:18takriban 5 BK

    Hakuna mtu yeyote aliyemwona Mungu wakati wowote, ila ni Mungu Mwana pekee, aliye kifuani mwa Baba ndiye ambaye amemdhihirisha.

  19. Yohana 1:19takriban 5 BK

    Huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati Wayahudi walipowatuma makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu kumuuliza, “Wewe ni nani?”

  20. Yohana 1:20takriban 5 BK

    Yohana alikiri waziwazi pasipo kuficha akasema, “Mimi si Kristo.”

  21. Yohana 1:21takriban 5 BK

    Wakamuuliza, “Wewe ni nani basi? Je, wewe ni Eliya?” Yeye akajibu, “Hapana, mimi siye.” “Je, wewe ni yule Nabii?” Akajibu, “Hapana.”

  22. Yohana 1:22takriban 5 BK

    Ndipo wakasema, “Basi tuambie wewe ni nani ili tupate jibu la kuwapelekea wale waliotutuma. Wewe wasemaje juu yako mwenyewe?”

  23. Yohana 1:23takriban 5 BK

    Akawajibu kwa maneno ya nabii Isaya, akisema, “Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Yanyoosheni mapito ya Bwana.’ ”

  24. Yohana 1:24takriban 5 BK

    Basi walikuwa wametumwa watu kutoka kwa Mafarisayo

  25. Yohana 1:25takriban 5 BK

    wakamuuliza, “Kama wewe si Kristo, wala si Eliya na wala si yule Nabii, kwa nini basi unabatiza?”