Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Sin: Tempt others to

8 mistari · 120 vipengele

Mistari kuhusu Tempt others to

  1. Mwanamke alipoona ya kuwa tunda la mti huo lilikuwa zuri kwa chakula na la kupendeza macho, tena linatamanika kwa kujipatia hekima, basi akachuma katika matunda yake, akala, pia akampa mumewe, aliyekuwa pamoja naye, naye akala.

  2. “Nilikuinua kutoka mavumbini na kukufanya kiongozi wa watu wangu Israeli, lakini ukaenenda katika njia za Yeroboamu na kusababisha watu wangu Israeli kutenda dhambi na kunikasirisha kwa dhambi zao.

  3. (Hapajapata kamwe kuwa na mtu kama Ahabu, aliyejiuza mwenyewe kutenda uovu machoni mwa Bwana, akiwa anachochewa na Yezebeli mkewe.

  4. Mwanangu, kama wenye dhambi wakikushawishi, usikubaliane nao.

  5. Kama wakisema, “Twende tufuatane; tukamvizie mtu na kumwaga damu, njoo tukavizie nafsi isiyo na hatia;

  6. tuwameze wakiwa hai kama kaburi, wakiwa wazima kama wale wanaotumbukia shimoni.

  7. Tutapata aina zote za vitu vya thamani na kujaza nyumba zetu kwa nyara.

  8. Njoo ushirikiane nasi, vitu vyote tutakavyopata tutagawana.”