Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Prayer

720 mistari · 120 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Ee Bwana, unijibu, kwa wema wa upendo wako; kwa huruma zako nyingi unigeukie.

  2. Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.

  3. Uwamwagie ghadhabu yako, hasira yako kali na iwapate.

  4. Walipize uovu juu ya uovu, usiwaache washiriki katika wokovu wako.

  5. Wafutwe kutoka kitabu cha uzima na wasiorodheshwe pamoja na wenye haki.

  6. Bwana huwasikia wahitaji wala hadharau watu wake waliotekwa.

  7. Wale wanaotafuta kuuondoa uhai wangu, waaibishwe na kufadhaishwa; wote wanaotamani kuangamizwa kwangu, warudishwe nyuma kwa aibu.

  8. Wale waniambiao, “Aha! Aha!” warudi nyuma kwa sababu ya aibu yao.

  9. Lakini bado mimi ni maskini na mhitaji; Ee Mungu, unijie haraka. Wewe ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu; Ee Bwana, usikawie.

  10. Washtaki wangu na waangamie kwa aibu, wale wanaotaka kunidhuru na wafunikwe kwa dharau na fedheha.

  11. Ee Mungu, usiniache, hata niwapo mzee wa mvi, mpaka nitangaze uwezo wako kwa kizazi kijacho, nguvu zako kwa wote watakaokuja baadaye.

  12. Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

  13. Ee Mungu, mtesi atakudhihaki mpaka lini? Je, adui watalitukana jina lako milele?

  14. Kwa nini unazuia mkono wako, mkono wako wa kuume? Uutoe kutoka makunjo ya vazi lako na uwaangamize!

  15. Ee Bwana, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki, jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.

  16. Likumbuke agano lako, maana mara kwa mara mambo ya jeuri yamejaa katika sehemu za giza nchini.

  17. Usiruhusu walioonewa warudi nyuma kwa aibu; maskini na wahitaji hebu walisifu jina lako.

  18. Inuka, Ee Mungu, ujitetee; kumbuka jinsi wapumbavu wanavyokudhihaki mchana kutwa.

  19. Usipuuze makelele ya watesi wako, ghasia za adui zako, zinazoinuka mfululizo.

  20. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa Yeduthuni. Zaburi ya Asafu. Nilimlilia Mungu ili anisaidie, nilimlilia Mungu ili anisikie.

  21. Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana, usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka na nafsi yangu ilikataa kufarijika.

  22. Kwa nini mataifa waseme, “Yuko wapi Mungu wenu?” Mbele ya macho yetu, dhihirisha kati ya mataifa kwamba unalipiza kisasi damu iliyomwagwa ya watumishi wako.

  23. Kilio cha huzuni cha wafungwa kifike mbele zako; kwa nguvu za mkono wako hifadhi wale waliohukumiwa kufa.

  24. Walipize jirani zetu mara saba vifuani mwao aibu walizovurumisha juu yako, Ee Bwana.

  25. Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?