Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Praise

490 mistari · 106 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Tuma hima nuru yako na kweli yako na viniongoze; vinilete mpaka mlima wako mtakatifu, mpaka mahali unapoishi.

  2. Ndipo nitakwenda madhabahuni pa Mungu, kwa Mungu, furaha yangu na shangwe yangu. Nitakusifu kwa kinubi, Ee Mungu, Mungu wangu.

  3. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Pigeni makofi, enyi mataifa yote, mpigieni Mungu kelele za shangwe!

  4. Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa, mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.

  5. Kwa kuwa Mungu ni mfalme wa dunia yote, mwimbieni zaburi za sifa.

  6. Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu, mlima wake mtakatifu.

  7. Atoaye dhabihu za shukrani ananiheshimu mimi, naye aiandaa njia yake ili nimwonyeshe wokovu wa Mungu.”

  8. Ee Bwana, fungua midomo yangu, na kinywa changu kitatangaza sifa zako.

  9. Nitakusifu milele kwa yale uliyoyatenda, nitatumaini jina lako, kwa kuwa jina lako ni jema. Nitakusifu mbele ya watakatifu wako.

  10. Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu,

  11. Ee Mungu, nina nadhiri kwako, nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani.

  12. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.

  13. Amka, nafsi yangu! Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.

  14. Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.

  15. Ee uliye Nguvu zangu, ninakuimbia sifa. Wewe, Ee Mungu, ndiwe ngome yangu, Mungu unipendaye.

  16. Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.

  17. Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.

  18. Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.

  19. Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.

  20. Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.

  21. Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Wimbo. Ee Mungu, sifa zakungojea katika Sayuni; kwako wewe nadhiri zetu zitatimizwa.

  22. Kwa mwimbishaji. Wimbo. Zaburi. Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote!

  23. Imbeni utukufu wa jina lake; mpeni sifa zake kwa utukufu!

  24. Dunia yote yakusujudia, wanakuimbia wewe sifa, wanaliimbia sifa jina lako.”

  25. Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, sauti ya sifa yake isikike,