- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Prayer
Mistari muhimu ya Biblia
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
Anapohukumiwa, apatikane na hatia, nayo maombi yake yamhukumu.
Watoto wake na waachwe yatima, mke wake na awe mjane.
Watoto wake na watangetange wakiomba, na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao.
Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni.
Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema wala wa kuwahurumia yatima wake.
Uzao wake na ukatiliwe mbali, majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho.
Maovu ya baba zake na yakumbukwe mbele za Bwana, dhambi ya mama yake isifutwe kamwe.
Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani.
Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo.
Alipenda kulaani, nayo laana ikampata; hakupenda kubariki, kwa hiyo baraka na ikae mbali naye.
Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.
Na iwe kama joho alilozungushiwa, kama mshipi aliofungiwa daima.
Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, kwa wale wanaoninenea mabaya.
Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, unitendee wema kwa ajili ya jina lako, uniokoe kwa wema wa pendo lako.
Maana mimi ni maskini na mhitaji, moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Ninafifia kama kivuli cha jioni, nimerushwa-rushwa kama nzige.
Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, mwili wangu umedhoofika na kukonda.
Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, wanionapo, hutikisa vichwa vyao.
Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, niokoe sawasawa na upendo wako.