Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Murmuring

170 mistari · 31 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?

  2. Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?

  3. Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.

  4. Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.

  5. Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

  6. Je, faraja za Mungu hazikutoshi, au maneno yaliyosemwa kwako kwa upole si kitu?

  7. Kwa nini moyo wako unakudanganya, na kwa nini macho yako yanangʼaa,

  8. ili kwamba upate kutoa hasira yako dhidi ya Mungu, na kumwaga maneno kama hayo kutoka kinywani mwako?

  9. “Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.

  10. Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?

  11. Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

  12. Zaburi ya Daudi. Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, wala usiwaonee wivu watendao mabaya,

  13. Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu.

  14. Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara.

  15. Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa.

  16. Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao.

  17. Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka.

  18. Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao.

  19. Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele,

  20. kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi.

  21. Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako.

  22. Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako.

  23. Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene.

  24. Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni,

  25. je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo?