Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Murmuring

170 mistari · 31 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.

  2. Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele.

  3. Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu?

  4. Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi.

  5. Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

  6. Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.

  7. Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.

  8. Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.

  9. Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.

  10. Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.

  11. Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.

  12. Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!

  13. Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.

  14. Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,

  15. nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.

  16. Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana.

  17. Kwa makusudi walimjaribu Mungu, wakidai vyakula walivyovitamani.

  18. Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani?

  19. Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, vijito vikatiririka maji mengi. Lakini je, aweza kutupa chakula pia? Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”

  20. Bwana alipowasikia, alikasirika sana, moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli,

  21. Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.

  22. Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,

  23. Niliamini, kwa hiyo nilisema, “Mimi nimeteseka sana.”

  24. Katika taabu yangu nilisema, “Wanadamu wote ni waongo.”

  25. Upumbavu wa mtu mwenyewe huharibu maisha yake hata hivyo moyo wake humkasirikia Bwana.