Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 2:12takriban 59 BK

    Basi hatukupokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, ili tuweze kuelewa kile kipawa ambacho Mungu ametupatia bure.

  2. 1 Wakorintho 2:13takriban 59 BK

    Haya ndiyo tusemayo, si kwa maneno tuliyofundishwa kwa hekima ya wanadamu bali kwa maneno tuliyofundishwa na Roho, tukifafanua kweli za kiroho kwa maneno ya kiroho.

  3. 1 Wakorintho 2:14takriban 59 BK

    Mtu ambaye hana Roho hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa upambanuzi wa rohoni.

  4. 1 Wakorintho 2:15takriban 59 BK

    Mtu wa kiroho hubainisha mambo yote, lakini yeye mwenyewe habainishwi na mtu yeyote.

  5. 1 Wakorintho 2:16takriban 59 BK

    “Kwa maana ni nani aliyefahamu mawazo ya Bwana ili apate kumfundisha?” Lakini sisi tunayo mawazo ya Kristo.

  6. 1 Wakorintho 3:1takriban 59 BK

    Ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama watu wa kiroho, bali kama watu wa mwilini, kama watoto wachanga katika Kristo.

  7. 1 Wakorintho 3:2takriban 59 BK

    Naliwanywesha maziwa, wala si chakula kigumu, kwa kuwa hamkuwa tayari kwa hicho chakula. Naam, hata sasa hamko tayari.

  8. 1 Wakorintho 3:3takriban 59 BK

    Ninyi bado ni watu wa mwilini. Kwa kuwa bado kuna wivu na magombano miongoni mwenu, je, ninyi si watu wa mwilini? Je, si mwaendelea kama watu wa kawaida?

  9. 1 Wakorintho 3:4takriban 59 BK

    Kwa maana mmoja anaposema, “Mimi ni wa Paulo,” na mwingine, “Mimi ni wa Apolo,” je, ninyi si wanadamu wa kawaida?

  10. 1 Wakorintho 3:5takriban 59 BK

    Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.

  11. 1 Wakorintho 3:6takriban 59 BK

    Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.

  12. 1 Wakorintho 3:7takriban 59 BK

    Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.

  13. 1 Wakorintho 3:8takriban 59 BK

    Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.

  14. 1 Wakorintho 3:9takriban 59 BK

    Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.

  15. 1 Wakorintho 3:10takriban 59 BK

    Kwa neema Mungu aliyonipa, niliweka msingi kama mjenzi stadi na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mmoja inampasa awe mwangalifu jinsi anavyojenga.

  16. 1 Wakorintho 3:11takriban 59 BK

    Kwa maana hakuna mtu yeyote awezaye kuweka msingi mwingine wowote isipokuwa ule uliokwisha kuwekwa, ambao ni Yesu Kristo.

  17. 1 Wakorintho 3:12takriban 59 BK

    Kama mtu yeyote akijenga juu ya msingi huu kwa kutumia dhahabu, fedha, vito vya thamani, miti, majani au nyasi,

  18. 1 Wakorintho 3:13takriban 59 BK

    kazi yake itaonekana ilivyo, kwa kuwa Siku ile itaidhihirisha. Itadhihirishwa kwa moto, nao moto utapima ubora wa kazi ya kila mtu.

  19. 1 Wakorintho 3:14takriban 59 BK

    Kama kile alichojenga kitabaki, atapokea thawabu yake.

  20. 1 Wakorintho 3:15takriban 59 BK

    Kama kazi kitateketea, atapata hasara, ila yeye mwenyewe ataokolewa, lakini tu kama mtu aliyenusurika kwenye moto.

  21. 1 Wakorintho 3:16takriban 59 BK

    Je, hamjui ya kwamba ninyi wenyewe ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

  22. 1 Wakorintho 3:17takriban 59 BK

    Kama mtu yeyote akiliharibu hekalu la Mungu, Mungu atamwangamiza; kwa maana hekalu la Mungu ni takatifu, na ninyi ndiyo hilo hekalu.

  23. 1 Wakorintho 3:18takriban 59 BK

    Msijidanganye. Kama mtu yeyote miongoni mwenu akidhani kuwa ana hekima kwa viwango vya dunia hii, inampasa awe mjinga ili apate kuwa na hekima.

  24. 1 Wakorintho 3:19takriban 59 BK

    Kwa maana hekima ya ulimwengu huu ni upuzi mbele za Mungu. Kama ilivyoandikwa: “Mungu huwanasa wenye hekima katika hila yao,”

  25. 1 Wakorintho 3:20takriban 59 BK

    tena, “Bwana anajua kwamba mawazo ya wenye hekima ni ubatili.”