Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. 1 Wakorintho 3:21takriban 59 BK

    Hivyo basi, mtu asijivune kuhusu wanadamu! Vitu vyote ni vyenu,

  2. 1 Wakorintho 3:22takriban 59 BK

    ikiwa ni Paulo au Apolo au Kefa au dunia au uzima au mauti, au wakati uliopo au wakati ujao, haya yote ni yenu

  3. 1 Wakorintho 3:23takriban 59 BK

    na ninyi ni wa Kristo, naye Kristo ni wa Mungu.

  4. 1 Wakorintho 4:1takriban 59 BK

    Basi, watu na watuhesabu sisi kuwa tu watumishi wa Kristo na mawakili wa siri za Mungu.

  5. 1 Wakorintho 4:2takriban 59 BK

    Tena, litakiwalo ni mawakili waonekane kuwa waaminifu.

  6. 1 Wakorintho 4:3takriban 59 BK

    Lakini kwangu mimi ni jambo dogo sana kwamba nihukumiwe na ninyi au na mahakama yoyote ya kibinadamu. Naam, hata mimi mwenyewe sijihukumu.

  7. 1 Wakorintho 4:4takriban 59 BK

    Dhamiri yangu ni safi, lakini hilo halinihesabii kuwa asiye na hatia. Bwana ndiye anihukumuye.

  8. 1 Wakorintho 4:5takriban 59 BK

    Kwa hiyo msihukumu jambo lolote kabla ya wakati wake. Ngojeni mpaka Bwana atakapokuja. Yeye atayaleta nuruni mambo yale yaliyofichwa gizani, na kuweka wazi nia za mioyo ya wanadamu. Wakati huo kila mmoja atapokea sifa anayostahili kutoka kwa Mungu.

  9. 1 Wakorintho 4:6takriban 59 BK

    Basi ndugu zangu, mambo haya nimeyafanya kwangu binafsi na Apolo kwa faida yenu, ili mweze kujifunza kutoka kwetu maana ya ule usemi usemao, “Msivuke zaidi ya yale yaliyoandikwa.” Hivyo hamtajivunia mtu fulani na kumdharau mwingine.

  10. 1 Wakorintho 4:7takriban 59 BK

    Kwa maana ni nani aliyewafanya kuwa tofauti na wengine? Ni nini mlicho nacho ambacho hamkupokea? Nanyi kama mlipokea, kwa nini mnajivuna kama vile hamkupokea?

  11. 1 Wakorintho 4:8takriban 59 BK

    Sasa tayari mnayo yale yote mnayohitaji! Tayari mmekwisha kuwa matajiri! Mmekuwa wafalme, tena bila sisi! Laiti mngekuwa wafalme kweli ili na sisi tupate kuwa wafalme pamoja nanyi!

  12. 1 Wakorintho 4:9takriban 59 BK

    Kwa maana ninaona kwamba Mungu ametuweka sisi mitume katika nafasi ya mwisho kabisa, kama watu waliohukumiwa kufa kwenye uwanja wa tamasha, kwa sababu tumefanywa kuwa maonyesho kwa ulimwengu wote, kwa malaika na kwa wanadamu pia.

  13. 1 Wakorintho 4:10takriban 59 BK

    Kwa ajili ya Kristo sisi ni wajinga, lakini ninyi mna hekima sana ndani ya Kristo. Sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu. Tunadharauliwa, lakini ninyi mnaheshimiwa.

  14. 1 Wakorintho 4:11takriban 59 BK

    Mpaka saa hii tuna njaa na kiu, tu uchi, tumepigwa na hatuna makao.

  15. 1 Wakorintho 4:12takriban 59 BK

    Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili,

  16. 1 Wakorintho 4:13takriban 59 BK

    tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Mpaka sasa tumekuwa kama takataka ya dunia na uchafu wa ulimwengu.

  17. 1 Wakorintho 4:14takriban 59 BK

    Siwaandikii mambo haya ili kuwaaibisha, bali ili kuwaonya, kama wanangu wapendwa.

  18. 1 Wakorintho 4:15takriban 59 BK

    Hata kama mnao walimu 10,000 katika Kristo, lakini hamna baba wengi. Mimi nilikuwa baba yenu katika Kristo Yesu kwa kuwaletea Injili.

  19. 1 Wakorintho 4:16takriban 59 BK

    Basi nawasihi igeni mfano wangu.

  20. 1 Wakorintho 4:17takriban 59 BK

    Kwa sababu hii ninamtuma Timotheo, mwanangu mpendwa na mwaminifu katika Bwana. Yeye atawakumbusha kuhusu njia za maisha yangu katika Kristo Yesu, ambayo yanakubaliana na mafundisho yangu ninayofundisha katika kila kanisa.

  21. 1 Wakorintho 4:18takriban 59 BK

    Baadhi yenu mmekuwa na jeuri mkidhani kuwa sitafika kwenu.

  22. 1 Wakorintho 4:19takriban 59 BK

    Lakini kama Bwana akipenda, nitafika kwenu mapema, nami nitapenda kujua, si tu kile wanachosema hawa watu jeuri, bali pia kujua nguvu yao.

  23. 1 Wakorintho 4:20takriban 59 BK

    Kwa kuwa Ufalme wa Mungu si maneno matupu tu bali ni nguvu.

  24. 1 Wakorintho 4:21takriban 59 BK

    Ninyi amueni. Je, nije kwenu na fimbo, au nije kwa upendo na kwa roho ya upole?

  25. 1 Wakorintho 5:1takriban 59 BK

    Yamkini habari imeenea ya kuwa miongoni mwenu kuna uzinzi ambao haujatokea hata miongoni mwa watu wasiomjua Mungu: Kwamba mtu anaishi na mke wa baba yake.