Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Strife

158 mistari · 57 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

  2. moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

  3. shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

  4. Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.

  5. Kiburi huzalisha magomvi tu, bali hekima hupatikana kwa wale wanaozingatia ushauri.

  6. Mtu mwepesi wa hasira huchochea ugomvi, bali mtu mvumilivu hutuliza ugomvi.

  7. Mtu mpotovu huchochea ugomvi, nayo maongezi ya upuzi hutenganisha marafiki wa karibu.

  8. Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.

  9. Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.

  10. Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.

  11. Midomo ya mpumbavu humletea ugomvi na kinywa chake hualika kipigo.

  12. Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuridhika kuliko mji uliozungushiwa ngome, nayo mabishano ni kama malango ya ngome yenye makomeo.

  13. Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye, naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha.

  14. Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.

  15. Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.

  16. Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.

  17. Mfukuze mwenye dhihaka, na mvutano utatoweka; ugomvi na matukano vitakoma.

  18. Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye huzuni? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko? Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?

  19. Ni hao wakaao sana kwenye mvinyo, hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

  20. usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?

  21. Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.

  22. Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.

  23. Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.

  24. Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.

  25. Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.