Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Waebrania 5:1takriban 64 BK

    Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu anawekwa kuwawakilisha kwa mambo yanayomhusu Mungu, ili apate kutoa matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi.

  2. Waebrania 5:2takriban 64 BK

    Kwa kuwa yeye mwenyewe ni dhaifu, aweza kuwachukulia kwa upole wale wasiojua na kupotoka.

  3. Waebrania 5:3takriban 64 BK

    Hii ndiyo sababu inampasa kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na vivyo hivyo kwa ajili ya dhambi za watu.

  4. Waebrania 5:4takriban 64 BK

    Hakuna anayejitwalia heshima hii mwenyewe; ni lazima aitwe na Mungu, kama vile Aroni alivyoitwa.

  5. Waebrania 5:5takriban 64 BK

    Pia Kristo hakujitwalia utukufu yeye mwenyewe wa kuwa Kuhani Mkuu, bali Mungu alimwambia, “Wewe ni Mwanangu; leo mimi nimekuzaa.”

  6. Waebrania 5:6takriban 64 BK

    Pia mahali pengine asema, “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”

  7. Waebrania 5:7takriban 64 BK

    Katika siku za maisha ya Yesu hapa duniani, alimtolea maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, yeye awezaye kumwokoa na mauti, naye Mungu akamsikia kwa sababu ya kutii kwake kwa unyenyekevu.

  8. Waebrania 5:8takriban 64 BK

    Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utiifu kutokana na mateso aliyoyapata,

  9. Waebrania 5:9takriban 64 BK

    na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii.

  10. Waebrania 5:10takriban 64 BK

    Naye amewekwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.

  11. Waebrania 5:11takriban 64 BK

    Tunayo mengi ya kusema kuhusu habari ya ukuhani huu, lakini ni vigumu kuyaeleza, kwa sababu ninyi ni wazito wa kuelewa.

  12. Waebrania 5:12takriban 64 BK

    Kwa hakika, ingawa mpaka wakati huu ingewapasa kuwa walimu, bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za awali za kweli ya Neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu!

  13. Waebrania 5:13takriban 64 BK

    Kwa maana yeyote aishiye kwa kunywa maziwa bado yeye ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafundisho kuhusu neno la haki.

  14. Waebrania 5:14takriban 64 BK

    Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ambao kwa kujizoeza wamejifunza kupambanua kati ya mema na mabaya.

  15. Waebrania 6:1takriban 64 BK

    Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tukisonga mbele ili tufikie utimilifu, sio kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,

  16. Waebrania 6:2takriban 64 BK

    mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele.

  17. Waebrania 6:3takriban 64 BK

    Mungu akitujalia tutafanya hivyo.

  18. Waebrania 6:4takriban 64 BK

    Kwa kuwa ni vigumu kwa wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu,

  19. Waebrania 6:5takriban 64 BK

    ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao,

  20. Waebrania 6:6takriban 64 BK

    kisha wakianguka, kuwarejesha tena katika toba. Kwa kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili na kumdhalilisha hadharani, nayo ikawa hasara kwao.

  21. Waebrania 6:7takriban 64 BK

    Ardhi ile ipokeayo mvua inyeshayo juu yake mara kwa mara hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao kwa ajili yao yalimwa, nayo nchi hiyo hupokea baraka kutoka kwa Mungu.

  22. Waebrania 6:8takriban 64 BK

    Lakini ardhi ikizaa miiba na mibaruti, haina thamani na iko hatarini ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.

  23. Waebrania 6:9takriban 64 BK

    Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu wapendwa, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mema zaidi, mambo yale yahusuyo wokovu.

  24. Waebrania 6:10takriban 64 BK

    Mungu si mdhalimu: yeye hataisahau kazi yenu na upendo ule mlioonyesha kwa ajili yake katika kuwahudumia watakatifu na hata sasa mnaendelea kuwahudumia.

  25. Waebrania 6:11takriban 64 BK

    Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho,