Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Water

197 mistari · 84 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Mmoja wao alipokuwa anakata mti, shoka lilitumbukia kwenye maji. Akalia, “Ee bwana wangu, shoka lilikuwa la kuazima!”

  2. Mtu wa Mungu akauliza, “Je, liliangukia wapi?” Alipomwonyesha mahali penyewe, Elisha akakata kijiti na kukitupa mahali pale, nalo shoka likaelea.

  3. Matukio mengine ya utawala wa Hezekia, mafanikio yake yote, na jinsi alivyotengeneza bwawa na mfereji ambao ulileta maji katika mji, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?

  4. akafanya shauri na maafisa wake na mashujaa wake juu ya kuzuia maji kutoka chemchemi zilizo nje ya mji, nao wakamsaidia.

  5. Kisha nikaelekea mpaka Lango la Chemchemi na Bwawa la Mfalme, lakini hapakuwepo nafasi ya kutosha kwa ajili ya mnyama wangu kupita,

  6. Je, mafunjo yaweza kumea mahali pasipo na matope? Matete yaweza kustawi bila maji?

  7. lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.

  8. kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.

  9. Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,

  10. “Lakini wao ni povu juu ya maji; sehemu yao juu ya nchi imelaaniwa, hivyo hakuna hata mmoja aendaye kwenye shamba la mizabibu.

  11. Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.

  12. Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.

  13. Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,

  14. Nimemiminwa kama maji, mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. Moyo wangu umegeuka kuwa nta, umeyeyuka ndani yangu.

  15. Hunilaza katika malisho ya majani mabichi, kando ya maji matulivu huniongoza,

  16. Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi, wavutapo pinde zao, mishale yao na iwe butu.

  17. Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, tulipita kwenye moto na kwenye maji, lakini ulituleta kwenye nchi iliyojaa utajiri tele.

  18. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa “Yungiyungi.” Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, niokoe, kwa maana maji yamenifika shingoni.

  19. alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, akayafanya maji yatiririke kama mito.

  20. Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.

  21. yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.

  22. Alivaa kulaani kama vazi lake, nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, kwenye mifupa yake kama mafuta.

  23. mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,

  24. maji yaendayo kasi yangalituchukua.

  25. Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.