- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
circa 6 BC – AD 30
The Life of Jesus
The eternal Son of God enters history: born in Bethlehem, baptized in the Jordan, crucified at Golgotha, raised on the third day.
Mistari ya kipindi hiki
- Mathayo 5:36takriban 31 BK
Nanyi msiape kwa vichwa vyenu, kwa kuwa hamwezi kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.
- Mathayo 5:37takriban 31 BK
‘Ndiyo’ yenu iwe ‘Ndiyo,’ na ‘Hapana’ yenu iwe ‘Hapana.’ Lolote zaidi ya hili latoka kwa yule mwovu.
- Mathayo 5:38takriban 31 BK
“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’
- Mathayo 5:39takriban 31 BK
Lakini mimi nawaambia, msishindane na mtu mwovu. Lakini kama mtu akikupiga kwenye shavu la kuume, mgeuzie na la pili pia.
- Mathayo 5:40takriban 31 BK
Kama mtu akitaka kukushtaki na kuchukua joho lako, mwachie achukue na koti pia.
- Mathayo 5:41takriban 31 BK
Kama mtu akikulazimisha kwenda maili moja, nenda naye maili mbili.
- Mathayo 5:42takriban 31 BK
Mpe yeye akuombaye, wala usimgeuzie kisogo yeye atakaye kukukopa.
- Mathayo 5:43takriban 31 BK
“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Mpende jirani yako na umchukie adui yako.’
- Mathayo 5:44takriban 31 BK
Lakini ninawaambia: Wapendeni adui zenu na waombeeni wanaowatesa ninyi,
- Mathayo 5:45takriban 31 BK
ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu waovu na watu wema, naye huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
- Mathayo 5:46takriban 31 BK
Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mtapata thawabu gani? Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?
- Mathayo 5:47takriban 31 BK
Nanyi kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je, mnafanya nini zaidi ya wengine? Je, hata watu wasiomjua Mungu, hawafanyi hivyo?
- Mathayo 5:48takriban 31 BK
Kwa hiyo kuweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
- Mathayo 6:1takriban 31 BK
“Angalieni msitende wema wenu mbele ya watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu aliye mbinguni.
- Mathayo 6:2takriban 31 BK
“Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na watu. Amin nawaambia wao wamekwisha kupokea thawabu yao.
- Mathayo 6:3takriban 31 BK
Lakini ninyi mtoapo sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa kushoto usijue mkono wako wa kuume unachofanya,
- Mathayo 6:4takriban 31 BK
ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo Baba yako wa mbinguni, yeye aonaye sirini atakupa thawabu kwa wazi.
- Mathayo 6:5takriban 31 BK
“Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki, maana wao hupenda kusali wakiwa wamesimama katika masinagogi na kando ya barabara ili waonekane na watu. Amin nawaambia, wao wamekwisha kupata thawabu yao.
- Mathayo 6:6takriban 31 BK
Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye sirini atakupa thawabu yako.
- Mathayo 6:7takriban 31 BK
Nanyi mnaposali msiseme maneno kama wafanyavyo watu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa maneno yao.
- Mathayo 6:8takriban 31 BK
Msiwe kama wao, kwa sababu Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla hamjamwomba.
- Mathayo 6:9takriban 31 BK
“Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba: “ ‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe.
- Mathayo 6:10takriban 31 BK
Ufalme wako uje. Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.
- Mathayo 6:11takriban 31 BK
Utupatie riziki yetu ya kila siku.
- Mathayo 6:12takriban 31 BK
Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyokwisha kuwasamehe wadeni wetu.