Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu Praise

490 mistari · 106 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,

  2. kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.

  3. Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.

  4. Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.

  5. Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.

  6. Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.

  7. Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu

  8. Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.”

  9. Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.

  10. Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:

  11. “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.

  12. Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,

  13. kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani,

  14. kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:

  15. ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,

  16. kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:

  17. kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu

  18. katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.

  19. Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,

  20. “Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”

  21. Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.

  22. ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:

  23. Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.

  24. Nawaambieni, vivyo hivyo kutakuwa na furaha zaidi mbinguni kwa sababu ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa wenye haki tisini na tisa ambao hawana haja ya kutubu.”

  25. Vivyo hivyo, nawaambia, kuna furaha mbele ya malaika wa Mungu juu ya mwenye dhambi mmoja atubuye.”