Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu God

662 mistari · 46 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.

  2. Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.

  3. “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?

  4. Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?

  5. Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.

  6. Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.

  7. Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.

  8. Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.

  9. Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.

  10. “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?

  11. Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?

  12. Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.

  13. Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.

  14. Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”

  15. Bwana akamwambia Ayubu:

  16. “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”

  17. Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:

  18. “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.

  19. Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”

  20. Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:

  21. “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.

  22. “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?

  23. Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?

  24. Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.

  25. Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,