Skip to content

Mistari ya Biblia kuhusu God: Unclassified scriptures relating to

354 mistari · 46 vipengele

Mistari kuhusu Unclassified scriptures relating to

Chuja kwa kitabu
  1. “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.

  2. Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.

  3. Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.

  4. Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.

  5. Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.

  6. Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.

  7. Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.

  8. Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.

  9. Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.

  10. “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.

  11. Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.

  12. Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.

  13. Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.

  14. “Naam, najua hili ni kweli. Lakini mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?

  15. Ingawa mtu angetaka kushindana naye, asingaliweza kumjibu Mungu hata mara moja miongoni mwa elfu moja.

  16. Hekima yake ni kubwa sana na ana uwezo mwingi mno. Ni nani aliyempinga naye akawa salama?

  17. Aiondoa milima bila yenyewe kujua na kuipindua kwa hasira yake.

  18. Aitikisa dunia kutoka mahali pake na kuzifanya nguzo zake zitetemeke.

  19. Husema na jua, nalo likaacha kuangaza; naye huizima mianga ya nyota.

  20. Yeye peke yake huzitandaza mbingu na kuyakanyaga mawimbi ya bahari.

  21. Yeye ndiye Muumba wa nyota za Dubu, na Orioni, Kilimia, na makundi ya nyota za kusini.

  22. Hutenda maajabu yasiyopimika, miujiza isiyoweza kuhesabiwa.

  23. Anapopita karibu nami, siwezi kumwona; apitapo mbele yangu, simtambui.

  24. Anapochukua kwa ghafula, ni nani awezaye kumzuia? Ni nani awezaye kumwambia, ‘Unafanya nini?’

  25. Mungu hataizuia hasira yake; hata jeshi kubwa la Rahabu lenye nguvu linajikunyata miguuni pake.