Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu God

662 mistari · 46 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?

  2. “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?

  3. Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?

  4. Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?

  5. Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni

  6. wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?

  7. “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa

  8. wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?

  9. Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

  10. “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?

  11. Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?

  12. Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.

  13. Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.

  14. “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?

  15. Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.

  16. Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.

  17. Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.

  18. “Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?

  19. Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?

  20. Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?

  21. Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?

  22. “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.

  23. Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,

  24. bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.

  25. Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,