Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Warumi 10:18takriban 60 BK

    Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”

  2. Warumi 10:19takriban 60 BK

    Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”

  3. Warumi 10:20takriban 60 BK

    Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”

  4. Warumi 10:21takriban 60 BK

    Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”

  5. Warumi 11:1takriban 60 BK

    Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini.

  6. Warumi 11:2takriban 60 BK

    Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli?

  7. Warumi 11:3takriban 60 BK

    Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?”

  8. Warumi 11:4takriban 60 BK

    Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.”

  9. Warumi 11:5takriban 60 BK

    Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu.

  10. Warumi 11:6takriban 60 BK

    Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.

  11. Warumi 11:7takriban 60 BK

    Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu,

  12. Warumi 11:8takriban 60 BK

    kama ilivyoandikwa: “Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo, macho ili wasiweze kuona, na masikio ili wasiweze kusikia, hadi leo.”

  13. Warumi 11:9takriban 60 BK

    Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa, kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.

  14. Warumi 11:10takriban 60 BK

    Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.”

  15. Warumi 11:11takriban 60 BK

    Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu.

  16. Warumi 11:12takriban 60 BK

    Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.

  17. Warumi 11:13takriban 60 BK

    Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu

  18. Warumi 11:14takriban 60 BK

    ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao.

  19. Warumi 11:15takriban 60 BK

    Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa?

  20. Warumi 11:16takriban 60 BK

    Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.

  21. Warumi 11:17takriban 60 BK

    Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni,

  22. Warumi 11:18takriban 60 BK

    basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe.

  23. Warumi 11:19takriban 60 BK

    Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.”

  24. Warumi 11:20takriban 60 BK

    Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.

  25. Warumi 11:21takriban 60 BK

    Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.