Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Warumi 9:26takriban 60 BK

    tena, “Itakuwa hasa mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’ ”

  2. Warumi 9:27takriban 60 BK

    Isaya anapiga kelele kuhusu Israeli: “Ingawa idadi ya wana wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni mabaki yao tu watakaookolewa.

  3. Warumi 9:28takriban 60 BK

    Kwa kuwa Bwana ataitekeleza hukumu yake duniani kwa haraka na kwa ukamilifu.”

  4. Warumi 9:29takriban 60 BK

    Ni kama vile alivyotabiri Isaya akisema: “Kama Bwana Mwenye Nguvu Zote asingelituachia uzao, tungelikuwa kama Sodoma, tungelifanana na Gomora.”

  5. Warumi 9:30takriban 60 BK

    Kwa hiyo tuseme nini basi? Kwamba watu wa Mataifa ambao hawakutafuta haki, wamepata haki ile iliyo kwa njia ya imani.

  6. Warumi 9:31takriban 60 BK

    Lakini Israeli, ambao walijitahidi kupata haki kwa njia ya sheria, hawakuipata.

  7. Warumi 9:32takriban 60 BK

    Kwa nini? Kwa sababu hawakuitafuta kwa njia ya imani bali kwa njia ya matendo. Wakajikwaa kwenye lile “jiwe la kukwaza.”

  8. Warumi 9:33takriban 60 BK

    Kama ilivyoandikwa: “Tazama naweka katika Sayuni jiwe la kukwaza watu na mwamba wa kuwaangusha. Yeyote atakayemwamini hataaibika kamwe.”

  9. Warumi 10:1takriban 60 BK

    Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.

  10. Warumi 10:2takriban 60 BK

    Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.

  11. Warumi 10:3takriban 60 BK

    Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.

  12. Warumi 10:4takriban 60 BK

    Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.

  13. Warumi 10:5takriban 60 BK

    Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”

  14. Warumi 10:6takriban 60 BK

    Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’ ” (yaani ili kumleta Kristo chini)

  15. Warumi 10:7takriban 60 BK

    “au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’ ” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.)

  16. Warumi 10:8takriban 60 BK

    Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.

  17. Warumi 10:9takriban 60 BK

    Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.

  18. Warumi 10:10takriban 60 BK

    Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.

  19. Warumi 10:11takriban 60 BK

    Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”

  20. Warumi 10:12takriban 60 BK

    Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.

  21. Warumi 10:13takriban 60 BK

    Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”

  22. Warumi 10:14takriban 60 BK

    Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?

  23. Warumi 10:15takriban 60 BK

    Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”

  24. Warumi 10:16takriban 60 BK

    Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”

  25. Warumi 10:17takriban 60 BK

    Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.