Rukia maudhui

circa AD 48–96

Letters to the Churches

Paul and other apostles write to strengthen, correct, and encourage the scattered churches across the Roman world.

2,767 mistari · 21 vitabu vimehusishwa

Mistari ya kipindi hiki

Chuja kwa kitabu
  1. Warumi 12:11takriban 60 BK

    Msiwe wavivu, bali mwe na bidii katika roho mkimtumikia Bwana.

  2. Warumi 12:12takriban 60 BK

    Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi.

  3. Warumi 12:13takriban 60 BK

    Changieni katika mahitaji ya watakatifu, wakaribisheni wageni.

  4. Warumi 12:14takriban 60 BK

    Wabarikini wale wanaowatesa, barikini wala msilaani.

  5. Warumi 12:15takriban 60 BK

    Furahini pamoja na wenye kufurahi, lieni pamoja na wale waliao.

  6. Warumi 12:16takriban 60 BK

    Kaeni kwa amani ninyi kwa ninyi. Msijivune, bali mwe tayari kushirikiana na wanyonge. Wala msiwe watu wenye kujivuna kwamba mnajua kila kitu.

  7. Warumi 12:17takriban 60 BK

    Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Jitahidini ili mtende yaliyo mema machoni pa watu wote.

  8. Warumi 12:18takriban 60 BK

    Kama ikiwezekana, kwa upande wenu kaeni kwa amani na watu wote.

  9. Warumi 12:19takriban 60 BK

    Wapendwa, msilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu, maana imeandikwa: “Ni juu yangu kulipiza kisasi, nitalipiza,” asema Bwana.

  10. Warumi 12:20takriban 60 BK

    Badala yake: “Kama adui yako ana njaa, mlishe; kama ana kiu, mpe kinywaji. Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake.”

  11. Warumi 12:21takriban 60 BK

    Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.

  12. Warumi 13:1takriban 60 BK

    Kila mtu na atii mamlaka inayotawala, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu, nazo mamlaka zilizopo zimewekwa na Mungu.

  13. Warumi 13:2takriban 60 BK

    Kwa hiyo yeye anayeasi dhidi ya mamlaka inayotawala anaasi dhidi ya kile kilichowekwa na Mungu, nao wale wafanyao hivyo watajiletea hukumu juu yao wenyewe.

  14. Warumi 13:3takriban 60 BK

    Kwa kuwa watawala hawawatishi watu wale wanaotenda mema bali wale wanaotenda mabaya. Je, wataka usimwogope mwenye mamlaka? Basi tenda lile lililo jema naye atakusifu.

  15. Warumi 13:4takriban 60 BK

    Kwa maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa ajili ya mema. Lakini kama ukitenda mabaya, basi ogopa, kwa kuwa hauinui upanga bila sababu. Yeye ni mtumishi wa Mungu, mjumbe wa Mungu wa kutekeleza adhabu juu ya watenda mabaya.

  16. Warumi 13:5takriban 60 BK

    Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu iwezayo kutolewa, bali pia kwa ajili ya dhamiri.

  17. Warumi 13:6takriban 60 BK

    Kwa sababu hii mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu, ambao hutumia muda wao wote kutawala.

  18. Warumi 13:7takriban 60 BK

    Mlipeni kila mtu kile mnachodaiwa. Kama mnadaiwa kodi lipeni kodi, kama ni ushuru, lipeni ushuru, astahiliye hofu, mhofu, astahiliye heshima, mheshimu.

  19. Warumi 13:8takriban 60 BK

    Msidaiwe kitu na mtu yeyote, isipokuwa kupendana, kwa maana yeye ampendaye mwenzake, ameitimiza sheria.

  20. Warumi 13:9takriban 60 BK

    Kwa kuwa amri hizi zisemazo, “Usizini,” “Usiue,” “Usiibe,” “Usitamani,” na amri nyingine zote, zinajumlishwa katika amri hii moja: “Mpende jirani yako kama nafsi yako.”

  21. Warumi 13:10takriban 60 BK

    Upendo haumfanyii jirani jambo baya. Kwa hiyo upendo ndio utimilifu wa sheria.

  22. Warumi 13:11takriban 60 BK

    Nanyi fanyeni hivi, mkiutambua wakati tulio nao. Saa ya kuamka kutoka usingizini imewadia, kwa maana sasa wokovu wetu umekaribia zaidi kuliko hapo kwanza tulipoamini.

  23. Warumi 13:12takriban 60 BK

    Usiku umeendelea sana, mapambazuko yamekaribia. Kwa hiyo tuyaweke kando matendo ya giza na tuvae silaha za nuru.

  24. Warumi 13:13takriban 60 BK

    Basi na tuenende kwa adabu kama inavyopasa wakati wa mchana, si kwa kufanya karamu za ulafi na ulevi, si kwa ufisadi na uasherati, si kwa ugomvi na wivu.

  25. Warumi 13:14takriban 60 BK

    Bali jivikeni Bwana Yesu Kristo, wala msifikiri jinsi mtakavyotimiza tamaa za miili yenu yenye asili ya dhambi.