- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Psalms
Mistari muhimu ya Biblia
jua halitakudhuru mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,
Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.
Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi. Nilishangilia pamoja na wale walioniambia, “Twende nyumbani ya Bwana.”
Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama malangoni mwako.
Yerusalemu imejengwa vyema kama mji ambao umeshikamanishwa pamoja.
Huko ndiko makabila hukwea, makabila ya Bwana, kulisifu jina la Bwana kulingana na maagizo waliopewa Israeli.
Huko viti vya enzi vya hukumu hukaa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
Omba kwa ajili ya amani ya Yerusalemu: “Wote wakupendao na wawe salama.
Amani na iwepo ndani ya kuta zako na usalama ndani ya ngome zako.”
Kwa ajili ya ndugu zangu na marafiki, nitasema, “Amani iwe ndani yako.”
Kwa ajili ya nyumba ya Bwana Mungu wetu, nitatafuta mafanikio yako.
Wimbo wa kwenda juu. Ninayainua macho yangu kwako, kwako wewe ambaye kiti chako cha enzi kiko mbinguni.
Kama vile macho ya watumwa yatazamavyo mkono wa bwana wao, kama vile macho ya mtumishi wa kike yatazamavyo mkono wa bibi yake, ndivyo macho yetu yamtazamavyo Bwana Mungu wetu, mpaka atakapotuhurumia.
Uturehemu, Ee Bwana, uturehemu, kwa maana tumevumilia dharau nyingi.
Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi, dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.
Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.
Wimbo wa kwenda juu. Wa Solomoni. Bwana asipoijenga nyumba, wajengao hufanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji, walinzi wakesha bure.
Mnajisumbua bure kuamka mapema na kuchelewa kulala, mkitaabikia chakula: kwa maana yeye huwapa usingizi wapenzi wake.
Wana ni urithi utokao kwa Bwana, watoto ni zawadi kutoka kwake.
Kama mishale mikononi mwa shujaa ndivyo walivyo wana awazaao mtu katika ujana wake.