Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Psalms: Prophetic Psalms

49 mistari · 16 vipengele

Mistari kuhusu Prophetic Psalms

  1. Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?

  2. Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

  3. Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

  4. Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.

  5. Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

  6. “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

  7. Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.

  8. Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.

  9. Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

  10. Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

  11. Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.

  12. Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

  13. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, uniweke salama, kwa maana kwako nimekimbilia.

  14. Nilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu; pasipo wewe sina jambo jema.”

  15. Kwa habari ya watakatifu walioko duniani, ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

  16. Huzuni itaongezeka kwa wale wanaokimbilia miungu mingine. Sitazimimina sadaka zao za damu au kutaja majina yao midomoni mwangu.

  17. Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu; umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

  18. Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri, hakika nimepata urithi mzuri.

  19. Nitamsifu Bwana ambaye hunishauri, hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

  20. Nimemweka Bwana mbele yangu daima. Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume, sitatikisika.

  21. Kwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia; mwili wangu nao utapumzika salama,

  22. kwa maana hutaniacha kaburini, wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu.

  23. Umenijulisha njia ya uzima; utanijaza na furaha mbele zako, pamoja na furaha za milele katika mkono wako wa kuume.

  24. Zaburi ya wana wa Kora. Wimbo. Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;

  25. Bwana anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.