Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Psalms: Psalms of Affliction

315 mistari · 16 vipengele

Mistari kuhusu Psalms of Affliction

  1. Zaburi ya Daudi. Alipomkimbia mwanawe Absalomu. Ee Bwana, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!

  2. Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”

  3. Lakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

  4. Ninamlilia Bwana kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.

  5. Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.

  6. Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.

  7. Ee Bwana, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.

  8. Kwa maana wokovu watoka kwa Bwana. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

  9. Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi. Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.

  10. Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu kuwa aibu mpaka lini? Mtapenda udanganyifu na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

  11. Fahamuni hakika kwamba Bwana amewatenga wale wamchao kwa ajili yake; Bwana atanisikia nimwitapo.

  12. Katika hasira yako, usitende dhambi. Mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya mkiichunguza mioyo yenu.

  13. Toeni dhabihu zilizo haki; mtegemeeni Bwana.

  14. Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye kutuonyesha jema lolote?” Ee Bwana, tuangazie nuru ya uso wako.

  15. Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa kuliko watu waliopata nafaka na divai kwa wingi.

  16. Nitajilaza chini na kulala kwa amani, kwa kuwa wewe peke yako, Ee Bwana, waniwezesha kukaa kwa salama.

  17. Kwa mwimbishaji. Kwa filimbi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, tegea sikio maneno yangu, uangalie kupiga kite kwangu.

  18. Sikiliza kilio changu ili unisaidie, Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa maana kwako ninaomba.

  19. Asubuhi, unasikia sauti yangu, Ee Bwana; asubuhi naleta haja zangu mbele zako, na kusubiri kwa matumaini.

  20. Wewe si Mungu unayefurahia uovu, kwako mtu mwovu hataishi.

  21. Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, unawachukia wote watendao mabaya.

  22. Unawaangamiza wasemao uongo. Bwana huwachukia wamwagao damu na wadanganyifu.

  23. Lakini mimi, kwa rehema zako kuu, nitakuja katika nyumba yako, kwa unyenyekevu, nitasujudu kuelekea Hekalu lako takatifu.

  24. Niongoze katika haki yako, Ee Bwana, kwa sababu ya adui zangu, nyoosha njia yako mbele yangu.

  25. Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika, mioyo yao imejaa maangamizi. Koo lao ni kaburi lililo wazi, kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu.