- English
- King James KJV
- Complete Jewish CJB
- World English WEBM
- Berean Standard BSB
- American Standard ASV
- Geneva GNV
- Young's Literal YLT
- Douay-Rheims DRC
- International
- Shqip ALB
- العربية SVD
- বাংলা BN-IRV
- မြန်မာ Judson
- 简体文 CUV-S
- 繁體中文 CUV-T
- Čeština BKR
- Nederlands STVE
- Français LSG
- Deutsch SCH
- Ελληνικά Vamvas
- ગુજરાતી GU-IRV
- Hausa HCB
- עברית Hebrew
- हिन्दी HCV
- Magyar KAROLI
- Bahasa Indonesia INDO-TB
- Italiano Diodati
- 日本語 Kougo
- 한국어 Korean
- മലയാളം MAL
- मराठी MRCV
- Norsk DNB
- فارسی OPV
- Polski BG
- Português Almeida
- Română Cornilescu
- Русский Synodal
- Español RVG
- Kiswahili Neno
- Svenska SV1917
- Tagalog TAG-ADB
- தமிழ் TCV
- తెలుగు TSA
- ภาษาไทย THAI-KJV
- Українська Ohienko
- Tiếng Việt CADMAN
- Yorùbá YCB
Mistari ya Biblia kuhusu Psalms
Mistari muhimu ya Biblia
Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.