Rukia maudhui

Mistari ya Biblia kuhusu Psalms

896 mistari · 16 vipengele

Mistari muhimu ya Biblia

Chuja kwa kitabu
  1. mashamba na yashangilie, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake. Kisha miti yote ya msituni itaimba kwa furaha;

  2. itaimba mbele za Bwana kwa maana anakuja, anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu dunia kwa haki, na mataifa katika kweli yake.

  3. Bwana anatawala, nchi na ifurahi, visiwa vyote vishangilie.

  4. Mawingu na giza nene vinamzunguka, haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake cha enzi.

  5. Moto hutangulia mbele zake na huteketeza adui zake pande zote.

  6. Umeme wake wa radi humulika dunia, nchi huona na kutetemeka.

  7. Milima huyeyuka kama nta mbele za Bwana, mbele za Bwana wa dunia yote.

  8. Mbingu zinatangaza haki yake, na mataifa yote huona utukufu wake.

  9. Wote waabuduo sanamu waaibishwa, wale wajisifiao sanamu: mwabuduni yeye, enyi miungu yote!

  10. Sayuni husikia na kushangilia, vijiji vya Yuda vinafurahi kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.

  11. Kwa kuwa wewe, Ee Bwana, ndiwe Uliye Juu Sana kuliko dunia yote; umetukuka sana juu ya miungu yote.

  12. Wale wanaompenda Bwana na wauchukie uovu, kwa maana yeye hulinda maisha ya waaminifu wake na kuwaokoa kutoka mkononi mwa mwovu.

  13. Nuru huangaza wenye haki na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.

  14. Furahini katika Bwana, ninyi mlio wenye haki, lisifuni jina lake takatifu.

  15. Bwana anatawala, mataifa na yatetemeke; anakalia kiti cha enzi katikati ya makerubi, dunia na itikisike.

  16. Bwana ni mkuu katika Sayuni; ametukuzwa juu ya mataifa yote.

  17. Wanalisifu jina lako ambalo ni kuu na la kuogopwa: yeye ni mtakatifu!

  18. Mfalme ni mwenye nguvu na hupenda haki, wewe umethibitisha adili; katika Yakobo umefanya yaliyo haki na sawa.

  19. Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, na mkaabudu katika mahali pa kuwekea miguu yake; yeye ni mtakatifu.

  20. Mose na Aroni walikuwa miongoni mwa makuhani wake, Samweli alikuwa miongoni mwa walioliitia jina lake; walimwita Bwana, naye aliwajibu.

  21. Alizungumza nao kutoka nguzo ya wingu; walizishika sheria zake na amri alizowapa.

  22. Ee Bwana, wetu, ndiwe uliyewajibu, kwa Israeli ulikuwa Mungu mwenye kusamehe, ingawa uliadhibu matendo yao mabaya.

  23. Mtukuzeni Bwana Mungu wetu, mwabuduni kwenye mlima wake mtakatifu, kwa maana Bwana Mungu wetu ni mtakatifu.

  24. Zaburi ya Daudi. Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa.

  25. Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: utakuja kwangu lini? Nitatembea nyumbani mwangu kwa moyo usio na lawama.